• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWATAKA MAWAZIRI WA MICHEZO KANDA YA 4 AFRIKA KIKUZA MICHEZO

Posted on: May 4th, 2023


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Mawaziri wa michezo wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya Nne kuweka nguvu katika kuhakikisha wanakuza na kuendeleza michezo kwa Ukanda huo.

Amesema hayo leo Alhamisi wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Michezo wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya IV Jijini Arusha.

Amesema kuwa mawaziri hao wawekeze kwenye kujenga uwezo wa kitalaamu ili kuzalisha wanamichezo wanaoweza kuleta mageuzi kwenye Sekta ya Maendeleo ya Michezo na Maendeleo kupitia Michezo.

 “Tusikubali kushika mkia kila siku na wala tusikubali kurudi nyuma”.

Amesema kuwa lengo la kila taifa ni kuona timu yake inashinda makombe ya Kimataifa hasa Kombe la Dunia.

“Tukiamua kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo na ujuzi pamoja na kushirikiana tunaweza kufikia malengo makubwa kwenye sekta ya michezo”

“Tunapaswa kufika mahali pa kuona kuwa Tanzania ikishinda wote tumeshinda, Uganda ikishinda, wote tumeshinda, Ethiopia ikishinda wote tumeshinda. Tushirikiane ili tuwe mfano na kielekezo kwa Kanda nyingine za Mabaraza ya Michezo ya Umoja wa Afrika”.

Katika Hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amewataka wajumbe wa mkutano huo kuichagua Tanzania kuwa makao makuu ya Sekretarieti ya Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Ukanda wa IV.

Amewaeleza wajumbe hao kuwa Tanzania ina kila sababu ya kupigiwa kura ya ndiyo kutokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuipa hadhi sekta ya michezo nchini.

Amesema kuwa uwepo wa mageuzi makubwa katika diplomasia ya michezo ya kimataifa ambapo chini ya uongozi thabiti wa Serikali, timu za Taifa za Tanzania na vilabu zinafanya vizuri katika mashindano ya Kimataifa jambo hili linatia hamasa kwa wanachama kuona kuwa Tanzania inapiga hatua katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.

“Uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali kwenye Miundombinu ya Michezo ikiwemo ujenzi wa Viwanja Vikubwa na vizuri vya Michezo vinavyokidhi viwango vya Kimataifa vya CAF na FIFA. Mathalan, Uwanja wa Taifa wa Benjamin Mkapa ambao hutumiwa kwa Michezo ya Kitaifa na Kimataifa  ikiwemo Timu ya Taifa ya Brazili na Klabu ya Everton ambazo pia zimewahi kuutumia”

Katika Mkutano huo, Rais Dkt. Samia Aliwasilisha ujumbe maalumu kwa wajumbe na Mawaziri wa michezo wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya Nne kuichagua Tanzania kuwa makao makuu ya Sekretarieti ya Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Ukanda wa IV.

 “Niwahakikishie kuwa Tanzania inauzoefu wa kuwa makao makuu ya taasisi mbalimbali za kimataifa, na pia Tanzania ina miundombinu yote muhimu ambayo itaiwezesha baraza hilo kufanya kazi kwa ufanisi” Amesema Rais Samia.

Naye Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Balozi Dkt Pindi Chana amesema kuwa tasnia ya michezo ni kati ya sekta ambazo inatoa ajira kwa vijana wengi “sekta ya michezo kwenye nchi wanachama ilitunga sheria ili kuendeleza vipaji, michezo inaiunganisha Afrika kuwa moja”

Ameongeza kuwa wataendeleza mapitio ya sheria kanuni na taratibu ili kuendelea kuikuza sekta ya michezo kwa kuwa michezo ni biashara na chanzo cha uhakika cha ajira kwa vijana.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa