Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewasili mkoani Arusha leo 18 Juni, 2025 na kupokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda,
Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pamoja na viongozi wengine wa Serikali.Mhe. Majaliwa atafungua Mkutano Mkuu wa chama cha Madaktari nchini unaofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa kimataifa wa AICC Arusha.
Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa