• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WEKENI WAZI TAARIFA ZA MAJI-RC KIMANTA

Posted on: March 10th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Iddi Hassan Kimanta amewataka wadau wa maji katika Mkoa wa Arusha kuweka wazi taarifa zao za kiutendaji ili kutoa nafasi ya utatuzi wa changamoto kwa urahisi.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa maji wa Mkoa wa Arusha, kikao hicho kilichojumuisha sekta za umma na binafsi.

Kimanta amesema uwazi wa taarifa utarahisisha kila mdau kuwa na uwelewa wa pamoja wa kila sehemu na kurahisha kupata suluhu ya changamoto.

Amesema mpaka sasa hali ya upatikanaji maji katika Mkoa wa Arusha hasa vijijini bado ipo chini sana kwani Mkoa ulijiwekea malengo ya kusambaza maji vijijini kwa 85% ifikapo 2020, lakini mpaka sasa ni 69.5% ya upatikanaji wa maji vijijini ndio umetekelezwa kuanzia 2015-2020.

 Vijiji 304 ndivyo vimeshapata maji hadi kufikia mwaka 2020 na vijiji 86 bado havijapatiwa maji kati ya vijiji 390 vyote na serikali inaendelea kuongeza wigo wa upatikanaji wa maji katika vijiji hivyo.

Kimanta amesema bado malengo ya serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 Mkoa wa Arusha uwe umefikia 100% ya upatikanaji maji vijijini.

Amesisitiza kuwa changamoto ya maji niya kila mmoja hivyo amewataka wadau hao kuhakikisha wanatoka na mpango mkakati mkubwa wa kuwezesha wananchi kupata maji kwa haraka zaidi.

Akitoa taarifa ya upatikanaji wa maji kwa Mkoa wa Arusha Meneja wa wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini injinia Emmanuel Makaidi amesema, RUWASA imependekeza bajeti ya Bilioni 17 kwa mwaka 2020/2021 na mpaka Februari 2021 bilioni 7.4 sawa na 58.7% zimeshatumika.

Makaidi amesema mpaka sasa RUWASA Mkoa wa Arusha imeshatekeleza miradi 4 yenye thamani ya bilioni 4.6 na miradi 8 inatarajiwa kuanzishwa katika halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Arusha.

Akitoa neno katika kikao hicho mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha bwana Zeloth Steven amesema ni vizuri sheria ya maji ikafahamika kwa mapana na kina kwa wananchi ili kuwaongezea uwelewa.

Aidha amewataka wadau hao wa maji kuhakikisha wana simamia miradi yote ya maji kwa umakini sana kwani katika kampeni za mwaka 2020 kero kubwa kwa wananchi ilikuwa ni upatikanaji wa maji katika maeneo mengi.

RUWASA  Mkoa wa Arusha umefanya kikao chake cha kwanza cha wadau kwa lengo la kujitambulisha kwa wadau na kuweza kushirikiana katika mambo mbalimbali na wadau  hao  na kuweza kutatua changamoto zinazowakabili.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa