• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WIKI YA SHERIA ARUSHA; ZAIDI YA WANANCHI LAKI MOJA WAPATA ELIMU NA MSAADA WA SHERIA BURE

Posted on: February 1st, 2024


Na Daniel Gitaro


Zaidi ya wananchi laki 1.9 Mkoani Arusha, wamepata elimu kuhusu masuala ya sheria pamoja na msaada wa kisheria bila gharama na wengine kwa gharama kidogo, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyofanyika kuanzia 24 -30 Januari, 2024 na kuhitimishwa Februari 01, 2024.


Akizungumza wakati wa kilele cha Siku ya Sheria Tanzania, sherehe iliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Mhe. Joachim Tiganga amesema kuwa, idadi hiyo ya wananchi imefikiwa kwa njia mbalimbali, ikiwemo vyombo vya habari na kuonana ana kwa ana, huku watu 516 kati ya hao wakipatiwa msaada wa kisheria.


"Katika wiki hiyo, watu wenhi zaidi walijitokeza huku Sheria mbalimbali zikifundishwa, kutokana na idadi ya watu, tuliowahudumi mwaka huu,  tumevunja rekodi ya miaka iliyopita kwenye maadhimisho kama haya". Amesema Mhe. Tiganga.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella amesema kuwa, Taasisi zinazojihusisha na Haki Jinai zinapaswa  kutambua namna bora ya kuunganisha mifumo yao katika kuboresha kazi na kuleta tija na Muunganiko unaoweza kufanywa kwa kutumia TEHAMA na kuwa na manufaa zaidi kwa jamii zetu.


Hata hivyo Mhe. Mongella ameongeza kuwa, dhima ya siku ya sheria inamlenga mwananchi na wadau wa sheria kwa ujumla wake kuendana na kasi ya Mahakama ya Mtandao ambayo ndiyo dira ya Mahakama kwa sasa pamoja na kutambua na kuelewa mifumo mbalimbali iliyowekwa katika upatikanaji na utoaji haki jinai. 


 "Wananchi  wana nafasi kubwa zaidi ya kujitafutia kwanza taarifa muhimu kuhusu haki zao zinazopatikana katika Tovuti za Taasisi za Umma kwa kuwa Silaha bora ya kupigania Haki ni kuelewa upatikanaji wa hiyo Haki unayopigania ipo chini ya Sheria, Kanuni au Taratibu ipi". Amesisitiza.


Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Chapter ya Arusha, Wakili George Njooka, amesema kuwa kila Mtanzania mpenda haki anawajibu wa kuunga mkono na kuhakikisha kuwa nia njema, utashi na juhudi za Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha na kuboresha mifumo Taasisi na Taasisi za Haki Jinai Nchini zinatekelezwa kwa tija na ufanisi mkubwa.


"Sisi kama chama cha wanasheria nchini, tunauhakikishia Umma kuwa tumejidhatiti kimkakati ili kuhakikisha kwamba tunatoa mchango wa kitaalam kwa kadri itakavyohitajika ili kutekeleza kwa tija na ufanisi mkubwa mapendekezo yaliyotolewa ya tume ya haki jinai". Ameweka wazi.


Awali, Maadhimisho ya Siku ya Sheria mwaka 2024 yamebeba Kauli mbiu ya "Umuhimu wa Dhana ya Haki kwa Ustawi wa Taifa; Nafasi ya Mahakama na Wadau katika Kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai"


#arushafursalukuki 




                        
                       
                        </div>
                        <!-- /.right-sidebar-content -->
                        <!--/END RIGHT SIDEBAR CONTENTE SECTION-->
                    </div>



<div class=

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa