Halmashauri ya Wilaya ya Longido imeagizwa kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kutoka asilimia 96 hadi kufikia asilimia 100 pamoja na kuhakikisha wanakamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wakati ili wananchi wapate maendeleo
Agizo hilo limetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Missaile Albano Musa wakati wa kujadili mapitio ya hoja tisa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/24 ambapo halmashauri hiyo ilipata hati safi.
"Ongezeni juhudi za ukusanyaji wa mapato ya ndani ili mfikie malengo ya asilimia 100 lakini pia niwapongeze mwa kupata hati safi na tunawapongeza wataalam wetu ikiwemo mkaguzi mkuu wa ndani kwakuonyesha mabadiliko makubwa katika kupunguza hoja na kuambatanisha vielelezo". Amesema.
Naye Mkaguzi wa Nje Mkoa wa Arusha, Valence Rutakyamirwa ameagiza vifaa vya afya vya shilingi milioni107 kuletwa mapema ili wananchi waweze kupata huduma bora za afya kwenye vituo vilivyopo wilayani humo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Salum Kali ameipongeza serikali kwa kutoa fedha kwaaajili ya miradi ya maendeleo kwani wilaya hiyo ni mojawapo ya wilaya inayopitisha magari zaidi ya 500 ya chakula yanayokwenda nchi mbalimbali kupitia mpaka wa Namanga na uchumi kukua zaidi.
Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa