• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Maji

MAJUKUMU

1.To asssist,coordinate backstopping and monitor operation and maintenance for water supply schemes in LGA's.

2. To facilitate LGA's in developing guidelines for operation and maintenance of water supply schemes in the repsective community projects and private operated schemes.

3.To facilitate provision of technical expertise to LGA's to suppport communities,institutions and private sector in operation and maintenance of water supply schemes.

4.Monitor and supervison of implementation of projects.

5.To coordinate, review and give recommendations on designs submitted by LGA's for water supply projects infrastructures.

6.To ccordinate and harmonize approaches for water sector implementation and standards of engineering for Urban and Rural water supply.

7. Representation of the Ministry of water in interpreting the National Water Sector Policies andf guidelines for Urban and Rural Water Supply.

8. Facilitating,coordinating and advice LGA's in implementation of NRWSSP activities including appraisal of Districts projects,Procurement of services from Contractors and Consultants and application of Public Procurement Act and Regulations, Budgeting and Financial Management.

9. To facilitate provision of linkage between LGA's ,other relevant authorities and the MoW in the planning and development of water sector components.

10. To facilitate provision of technical expertise and advice to LGA's in capacity building and support for community owned water supply organisation (COWSOs) in operation and maintenance of water supply schemes.

11. Helping LGA's in preparing the guidelines for implementation and rehabilitation of water projects i.e Design of water projects,preparation of Bill of Quantities (BOQ),preparation of Tender documents,Evaluation of bids,preparation of contracts documents,supervision and coordination of Construction of water schemes, setting out and surveying,attending different Regional Meetings, Planning and Budgeting.

Hali ya huduma ya Maji 

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi waishio vijijini katika Mkoa wa Arusha imeendelea kuimarika siku kwa siku, mpaka sasa asilimia 70.2 ya wakazi waishio vijijini katika Mkoa wa Arusha wanapata huduma ya maji safi na salama kupitia miradi ya maji inayotoa huduma iliyopo. Aidha, jumla ya vijiji 304 kati ya 390 vinahuduma ya maji rasmi na vijiji 86 havina huduma rasmi ya maji. Serikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini imepanga kuvipatia huduma ya maji vijiji vyote visivyo na huduma rasmi ya maji ifikapo 2024, katika Mkoa wa Arusha.

Serikali kupitia RUWASA Mkoa wa Arusha katika kipindi cha bajeti 2021/2022 imeendelea kujenga miradi mipya,kukarabati na kupanua miundombinu ya usambazaji maji vijijini, ambapo jumla ya miradi 66 yenye thamani Tsh.32,610,648,952.64 inaendelea kutekelezwa na ipo hatua mbalimbali za utekelezaji, Aidha, miradi hii ikikamilika itapunguza idadi ya vijiji visivyo na huduma ya maji rasmi kutoka 86 hadi 63, na hivyo kuboresha hali ya huduma ya maji vijijini kwa kuongeza  upatikanaji wa huduma ya maji  kutoka asilimia 70.2 ya sasa hadi asilimia 76.2,  ifikapo Juni, 2022.

Katika bajeti ya 2021/2022 RUWASA Mkoa wa Arusha iliidhinishiwa jumla ya Tsh.10,276,348,023 Kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji vijijini, hadi sasa jumla ya Tsh.4,396,637,286.90 zimepokelewa sawa na asilimia 42.9 ya bajeti. Aidha, tulipokea bajeti ya ziada kiasi cha jumla ya Tsh. 2,470,881,598.03 kupitia program ya mpango wa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji 5 vijijini ambapo hadi sasa utekelezaji unaendelea katika hatua mbalimbali.

Katika usimamiaji wa huduma ya maji kwa skimu za maji  zilizokamilika, Mkoa wa Arusha kupitia RUWASA imeendelea na zoezi la uhuishaji na uundaji wa vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya jamii kama inavyoelekezwa na sheria ya huduma za maji Na.5 ya mwaka 2019, ili kuimarisha huduma ya maji vijijini na kuwa na uendelevu wa miradi ya maji. Hadi sasa jumla ya vyombo 97 kati ya 101 vimehuishwa na kusajiliwa kisheria kwa ajili ya kusimamia utoaji wa huduma ya maji ngazi ya jamii.

Hali ya Huduma ya Maji Mjini

Kuhusu utaoji wa huduma ya maji mijini, Serikali Mkoani Arusha inatekeleza miradi mbalimbali mikubwa ya kimkakati yenye lengo la kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji mijini kwa kiwango cha asilimia 100. Hivi sasa, miradi hiyo inaendelea kutekelezwa katika meneo mbalimbali kama ifuatavyo:

Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi mkubwa wa maji katika Jiji la Arusha kwa gharama ya Shilingi Bilioni 520 utakapokamilika. Mradi huu pamoja na shughuli nyingine unahusisha uchimbaji wa visima virefu 56 na unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa Jiji la Arusha kwa zaidi ya asilimia 100 ikiwa ni pamoja na:

Kuongeza kiwango cha kuzalisha maji kutoka wastani wa lita 40,000,000 hadi lita 200,000,000 kwa siku.

Kuongeza idadi ya wakazi wanaopata maji kutoka wastani wa 325,000 hadi kufikia 600,000 wakiwemo wastani wa watu 250,000 wanaoingia na kutoka Jijini kila siku.

Kupunguza upotevu wa maji kutoka wastani wa asilimia 40 hadi asilimia 25.

Kuongeza mtandao wa maji safi kutoka asilimia 44 ya sasa hadi asilimia 100;

Kuongeza mtandao wa kukusanya majitaka kutoka asilimia 7.66 hadi asilimia 30

Mpaka sasa, hali halisi ya utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 70 na umepangwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2022. Mamlaka imeweza kuongeza huduma ya upatikanaji majisafi na huduma ya uondoaji majitaka imeimarika katika Jiji la Arusha. Yafuatayo ni baadhi ya mafanikio na faida zilizopatikana baada ya utekelezaji wa mradi kuendelea: -

  • Kiwango cha uzalishaji maji kimeweza kuongezeka kwa lita 17,400,000 kwa siku. Kiasi hiki cha maji kimeongezeka baada ya Menejimenti kuweka mpango wa dharura kuhakikisha wananchi wanapata maji baada ya Mradi wa uchimbaji wa Visima virefu 11 katika eneo la SeedFarm kukamilika. Upatikanaji wa maji kutoka kwenye eneo la SeedFarm limeweza kuwahudumia wananchi katika maeneo yaliyokuwa na uhaba wa maji hasa katika maeneo ya Murrieti, Olasiti, Sombetini kwa Morombo, Olmoti, Sokoni 1, na baadhi ya maeneo ya Terrat.
  • Kufanya maunganisho mapya 444 ya wateja wa maji taka katikati ya mji (CBD) na wateja 1,521 nje ya CBD, Pamoja na kuhamisha wateja 2,961 wa huduma ya majisafi kutoka kwenye mtandao wa zamani na kuwaunganisha kwenye mtandao mpya wa maji safi katika eneo la CBD.
  • Kufanya ukarabati na upanuzi wa mtandao wa maji safi na mtandao wa maji taka katikati ya Jiji la Arusha. Mtandao wa maji safi umefanyiwa ukarabati na upanuzi wa 48.61 km wakati mtandao wa maji taka ukarabati na upanuzi wa mtandao umefanyika kwa 27.47 km, vilevile kupitia mradi Mamlaka imeweza kujenga chemba za ukaguzi (Manholes) 603 katika eneo la CBD na Manhole 4,024 nje ya eneo la CBD katika mfumo wa maji taka.
  • Maji taka kutoka eneo la CBD yameanza kuingia kwenye mfumo mpya wa kutibu maji taka baada ya ujenzi wa mabwawa 18 Terrat kukamilika kwa asilimia 100.
  • Kufunga mtambo wa kupima utendaji wa Dira “Water Mete Testing Bench” katika eneo la Loruvan Yard. Mtambo huu utasaidia kuondoa kero za malalamiko ya wateja kuhusu ufanisi wa utendaji kazi wa dira zao.
  • Upatikanaji wa ajira kwa watu takribani 2,000 ikiwa ni watu 200 kutoka nje ya nchi na 1,800 kutoka ndani ya nchi na kati ya hao 700 wakiwa ni waajiriwa kwenye ujuzi mbalimbali.
  • Ununuzi wa vifaa kwenye viwanda vya ndani na maduka ya jumla ya shilingi za Kitanzania Bilioni 113.0.
  • Manufaa kwa wananchi wapatao 1,037 kwa kuwalipa fidia kiasi cha Shilingi Bilioni 5.687 kwa kutoa maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu.
  • Mradi pia katika kuzingatia masuala ya usafi wa mazingira, umejenga vyoo katika maeneo mbalimbali ya umma (Shule za Msingi 16, Shule za Sekondari 2, Zahanati 2, Masoko 3, Ofisi ya kata 1 na Maeneo ya wazi 1). Jumla ni maeneo 25.
  • Dira za maji za zamani kwa wateja takribani 25,000 zimebadilishwa na hivyo kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.
  • Matanki 9 kati ya 11 yanayopaswa kujengwa yamekamilika na kati ya hayo, matanki manne (4) yenye uwezo wa kuhifadhia maji kiasi cha lita 17,000,000 yameanza kutumika.

 Mahitaji ya maji katika Miji midogo Mkoa wa Arusha 

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji mdogo wa Longido lita 1,501,000, Mji mdogo wa Ngaramtoni lita 7,444,240, Mji mdogo wa Monduli lita 2,038,890 na Mji mdogo wa USA River lita 4,114,500) wakati maji yanayozalishwa ni lita 70,000,000 kwa siku sawa na asilimia 63.8% ya mahitaji kwa siku.

Matarajio ni kufikia asilimia 100 ifikapo mwezi Juni, 2025 baada ya kukamilika kwa miradi inayoendelea kutekelezwa. Mamlaka imepanga kuongeza mtandao wa majisafi kwa zaidi ya kilomita 453.829 katika maeneo mbalimbali (lengo ni kuongeza kilomita 200 jiji la Arusha, kilomita 30.561 mji wa Ngaramtoni, kilomita 95 mji wa Monduli, kilomita 73.268 mji wa USA River na kilomita 55 mji wa Longido). Ongezeko hili la mtandao litapelekea huduma ya majisafi kuongezeka kutoka asilimia 72.3 ya sasa na kufika asilimia 100. Aidha, Mamlaka imepanga kufanya maunganisho mapya kwa wateja 41,978 hadi kufikia mwaka 2025/26, ambapo utekelezaji wa mpango huo umeanza.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa