• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Elimu

Sekta ya elimu katika mkoa wetu inaendelea kuimarika kwakasi kubwa kuanzia ngazi ya awali hadi vyuo.

Mkoa wa Arusha kwa mwaka 2018 umeweza kushika nafasi mbalimbali Kitaifa kama ifuatavyo;

-Darasa la nne nafasi ya 3 Kitaifa  mwaka 2020

-Darasa la Saba nafasi ya 2 Kitaifa mwaka 2020

-Kidato cha Pili nafasi ya 1 Kitaifa mwaka 2020

-Kidato cha nne nafasi ya 1 Kitaifa mwaka 2020

Kidato cha Sita nafasi ya 6 Kitaifa mwaka 2020


Halmashauri zilizofanya vizuri 2020

Darasa la Nne

Halmashauri ya Jiji la Arusha ya kwanza katika Halmashauri Kitaifa

Darasa la Saba

Halmashauri ya Arusha Jiji ya kwanza Kitaifa

Halmashauri ya Arusha ya Nane katika halmashauri kumi bora Kitaifa

Kidato cha Pili

Halmashauri ya Arusha Jiji  na Halmashauri ya Arusha zipo katika Halmashauri kumi bora

Kidato cha Nne

Halmashauri ya Meru imeingia kumi bora Kitaifa

Kidato cha Sita

Shule 3 zimeingia katika kumi bora

1.Kisimiri

2.Ilboru

3.Mwandet

Mkoa wa Arusha una jumla ya taasisi za kielimu 1,082 zinazotoa Elimu kuanzia Elimu ya Awali hadi Elimu ya Juu. Kati ya hizo zipo shule za msingi za umma na za binafsi 757, Sekondari 240, vyuo vya ualimu 10, Vyuo vya ufundi stadi 52, vyuo vikuu 9 na Vyuo vinginevyo 14.

Katika kuimarisha sekta ya elimu Serikali imeendelea kutekeleza mikakati anuawai yenye lengo la kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunza na pia mikakati yenye kuzilenga kaya maskini sana (poor of the poor). Hii ni pamoja na uanzishwaji wa shule mpya, ujenzi wa miundombinu ya elimu na upatikanaji wa vifaa, kuanzishwa kwa mpango wa elimu bila malipo na mpango wa elimu lipa kwa matokeo. Hatua zilizochukuliwa kupitia mikakati hiyo ni kama ifuatavyo:

  • Mikakati ya Serikali

 

  • Ujenzi wa shule mpya

Hadi kufikia mwezi Juni 2019 Serikali Mkoani Arusha imeweza kuongeza idadi ya shule za msingi kutoka shule 519 mwaka 2015 na kufikia shule 537 mwaka 2019, kukiwa na ongezeko la shule mpya 18 sawa na asilimia 3.5. Shule za msingi za binafsi zilizopo ni 245 na hivyo kufanya idadi ya shule zote kuwa ni 782.

Shule za Sekondari za umma zimeongezeka kutoka 142 mwaka 2015 hadi 155 mwaka 2019, kukiwa na ongezeko la shule mpya 13, sawa na asilimia 9.2. Shule za Sekondari za binafsi zilizopo ni 99 na kufanya Mkoa kuwa na shule za sekondari 254.

  • Mpango wa Elimu bila Malipo

Mpango wa Elimu bila Malipo ni mahsusi katika kuhakikisha kuwa kila mototo wa Tanzania anapata fursa ya Elimu ya Msingi (hadi kidato cha Nne) bila vikwazo vya kiuchumi au kijamii. Chini ya Mpango huo, Serikali imetoa jumla ya Shilingi 78,283,011,450 kwa Mkoa wa Arusha kati ya mwaka 2016 na 2019 ikiwa ni wastani wa Shilingi bilioni 1.80 kwa mwezi. Matumizi ya fedha hizi ni pamoja na:

  • Uendeshaji wa shule (mitihani ya shule;
  • Ununuzi wa  vifaa  na vitabu vya kufundishia;
  • Shughuli za ukarabati mdogo mdogo;
  • Gharama za chakula kwa ajili ya shule za bweni na vitengo vya wanafunzi wa elimu maalum;
  • Ununuzi wa vifaa vya maabara, na;
  • Malipo ya posho ya madaraka kwa walimu wakuu wa shule na waratibu elimu kata.

Kwa wastani, jumla ya wanafunzi 416,773 wamekuwa wakinufaika na Mpango wa Elimu bila Malipo kila mwaka.

  • Ujenzi wa Maabara katika shule za Sekondari 

Katika kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari Serikali imeendelea kuwekeza katika ujenzi wa maabara kwa masomo ya Bailojia, Fizikia na Kemia. Kutokana na sera hiyo Serikali Mkoani Arusha imeweza kuongeza idadi ya vyumba vya maabara kutoka 49 mwaka 2015 hadi kufikia maabara 364 mwaka 2019 ikiwa ni ongezeko la maabara 315 sawa na asilimia 643!. Hivi sasa Serikali inaendelea na uimarishaji wa maabara hizo kwa kuhakikisha zinakuwa na vifaa vyote muhimu kwa ajili ya wanafunzi kujifunzia.

  • Ukamilishaji wa Miradi ya Wananchi (Maboma)

Mkakati huu wa Serikali unalenga kutambua mchango unaotokana na juhudi za wananchi na pia kupanua wigo wa wao kushiriki katika kuimarisha sekta ya elimu nchini. Katika kutekeleza kipaumbele hiki, Serikali imetumia jumla ya TZS 1,575,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi ya madarasa yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi katika shule za sekondari na shule za msingi ambapo jumla ya madarasa 78 na vyoo matundu 238 yamejengwa katika shule za msingi na madarasa 78 katika shule za sekondari.

  • Mpango wa Elimu wa Lipa Kwa Matokeo (EP4R).

Mpango wa Elimu wa Lipa kwa Matokeo ni utaratibu unaohusu upimaji wa ufanisi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kutumia vigezo muhimu vya kielimu kama urekebishaji wa ikama ya walimu, uingizaji wa takwimu za kielimu zilizo sahihi kwenye mfumo wa BEMIS (Basic Education Management Information System) na hivyo kuziwezesha kupatiwa fedha kulingana na ubora wa matokeo ya upimaji.

Tangu kuanza kwa Mpango huo mwaka 2015/2016 Mkoa wa Arusha umepokea jumla ya Shilingi 5,765,713,767 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa, mabweni, mabwalo, matundu ya vyoo na ukamilishaji wa miradi ya ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari na pia kulipa motisha kwa walimu wanaofanya vizuri kwenye utendaji kazi wao.

Kati ya fedha hizo, jumla ya TZS 1,203,200,000 zimetumika kwenye shule za sekondari kwa shughuli za ujenzi wa ofisi za utawala 3, matundu ya vyoo 12, mabwalo 2, maktaba 2, mabweni 8, madarasa 9 na nyumba 1. Kiasi kilichosalia cha TZS 651,000,000 kilitumiwa na shule za msingi kujenga madarasa 20, matundu ya vyoo 66, bweni 1 na nyumba 3 za walimu.

  • Uendeshaji wa Mitihani ya Pamoja

Katika kuimarisha ufaulu wa wanafunzi katika ngazi zote za elimu ya msingi na sekondari, Mkoa wa Arusha umeanzisha Mpango maalum wa kufanya mitihani ya pamoja ya ndani ya kuwapima wanafunzi kwa shule zote kabla ya mitihani ya kitaifa. Utaratibu huu unaosimamiwa moja kwa moja na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha ambapo tathmini za awali zimeonyesha kuwepo kwa ari ya kufundisha, kwa mujibu wa syllabus miongoni mwa walimu ili kujihakikishia matokeo mazuri.

  • Mafanikio yaliyopatikana

Mafanikio yaliyopatikana kutokana na juhudi hizo za Serikali ni pamoja na:

  • Ongezeko la Uandikishaji wa Wanafunzi

Kumekuwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa ngazi mbalimbali za elimu hususan kutokana na mpango wa Serikali wa Elimu bila malipo:

  • Uandikishaji wa elimu ya awali – uandikishaji kwa mwaka 2019 ulikuwa ni 47,711 ikilinganishwa na wanafunzi 31,198 mwaka 2015 ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 16,513, sawa na asilimia 53.
  • Uandikishaji darasa la kwanza - Wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza kwa mwaka 2019 ni 53,324, ikilinganishwa na wanafunzi 43,068 walioandikishwa mwaka 2015, ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 10,256 sawa na asilimia 24.
  • Uandikishaji kidato cha kwanza – wanafunzi walioandikishwa kwa mwaka 2018/19 ni 33,935 ikilinganishwa na wanafunzi 27,005 walioandikishwa mwaka 2015. Hili ni ongezeko la wanafunzi 6,930 sawa na asilimia 26.
  •  

Ongezeko la Kiwango cha Ufaulu 

Maendeleo ya ufaulu wa wanafunzi katika ngazi mbalimbali za elimu, kati ya mwaka 2015 na mwaka 2019 ni kama ifuatavyo:

  • Ufaulu Darasa la Saba – kiwango cha ufaulu kimeongezeka kutoka asilimia 79.67 mwaka 2015 hadi asilimia 87.30 mwaka 2018 na kufanya Mkoa kushika nafasi ya Tatu kitaifa.
  • Ufaulu kidato cha Pili – kiwango cha ufaulu mwaka 2018 kiliongezeka na kufikia asilimia 94.5 ikilinganishwa na asilimia 92 mwaka 2016, na kufanya Mkoa wa Arusha ulishika nafasi ya Kwanza kitaifa.
  • Ufaulu kidato cha Nne – katika mwaka 2018 ulikuwa ni asilimia 82.4 ikilinganishwa na asilimia 67.5 mwaka 2016, ambapo Mkoa ulishika nafasi ya Tatu kitaifa.
  • Mafanikio mengine 

Mafanikio mengine yaliyopatikana ni pamoja na:

  • Kuanzishwa kwa madarasa ya Elimu ya Awali 398 katika shule za msingi;
  • Mdondoko wa wanafunzi katika Elimu Msingi umepungua kutoka asilimia 6.9 hadi kufikia asilimia 2.1;
  • Wanafunzi wanaomaliza mzunguko wa elimu katika Elimu Msingi wameongezeka kutoka asilimia 80.2 hadi asilimia 95.6

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa