• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

BILIONI 14.4 KULIPWA FIDIA, UTEKELEZAJI MRADI WA MAGADI SODA WILAYANI MONDULI.

Posted on: January 23rd, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa Jumla ya Shilingi Bilioni 14.4 kama fidia kwa Wakazi wa Vijiji vinne vilivyopo kwenye Kata ya Engaruka Wilayani Monduli Mkoani Arusha ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa Serikali ya awamu ya sita katika uendelezaji wa miradi ya Kimkakati yenye tija kwa Taifa.



Kwaniaba ya Rais Samia leo Alhamisi Januari 23, 2025, Waziri wa Viwanda na biashara Mhe. Dkt. Seleman Jaffo wakati akizindua ugawaji wa fidia hizo kwa awamu ya kwanza yenye takribani Bilioni 6.2, amewataka wasimamizi wa zoezi hilo kuhakikisha kuwa ulipaji wa fidia hizo unamalizika kabla ya Februari 15, 2025, na kuaigiza shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kushughulikia malalamiko yote ya ya fidia kwa wananchi wa eneo hilo.



Katika hatua nyingine Waziri Jafo aliyeambatana na Viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Wizara ya ardhi Mhe. Jofrey Pinda, amesema serikali imeweka mpango maalum wa kuhakikisha kuwa eneo la Engaruka linakuwa na barabara zinazopitika muda wote sambamba na upatikanaji wa umeme mkubwa wa Kilowati 33 ili kusaidia katika shughuli za uendeshaji wa viwanda viwili vikubwa vinavyotarajiwa kutekeleza mradi huo.



Akizungumza katika Uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda, amesema Arusha ni miongoni mwa mikoa yenye bahati na kadri siku zinavyosonga, Mkoa huu utatoa fursa mbalimbali za maendeleo kwenye sekta za Kilimo, Madini na Michezo, zitakazosaidia wananchi kujikwamua na umaskini akihimiza kuendelea kupewa kipaumbele cha ajira kwa wazawa wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Mkoa wa Arusha.



Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo wa Kimkakati, Mkurugenzi mwendeshaji wa NDC Dkt.Nicolaus Shombe amesema mradi huo wa magadi soda umechukua zaidi ya miaka 29 tangu mchakato wake ulipoanza baada ya NDC kufanya utafiti wake na kubaini uwepo wa magadisoda yenye kufikia mita za ujazo Bilioni 3.8 sawa na tani Milioni 787 ambapo kupitia utekelezaji wake, viwanda viwili vikubwa vitakavyogharimu Trilioni 1.6 vitajengwa katika eneo hilo lenye jumla ya ekari 60, 884.

May be an image of 8 people, lighting, dais and text

May be an image of 6 people and people dancing

May be an image of one or more people, crowd and text

May be an image of 2 people, dais and text

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa