• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YA AWAMU YA SITA INA IMANI KUBWA SANA NA WALIMU NCHINI: RAIS SAMIA..

Posted on: December 18th, 2023

OR - TAMISEMI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali itaendelea kuboresha Maslahi ya Walimu ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba za Makazi kwenye vituo vyao vya kazi ili kuwawekea mazingira nadhifu ya kazi.


Mhe. Rais amesema hayo leo Disemba 17, 2023 wakati akiongea na Jumuiya ya Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) kwa njia ya Simu wakati wa Mkutano uliowakutanisha zaidi ya wajumbe 3500 kwenye Ukumbi wa Kwatunza Beach Resort Mkoani Mwanza  wakati Waziri wa TAMISEMI akifunga Mkutano huo wa 18 wa Mwaka.


"Serikali ina imani sana na Walimu nchini na kwakweli tupo tayari kuboresha mazingira yenu ya Kazi na katika kutekeleza hilo tunalifanyia kazi suala la Maslahi yenu katika mambo mbalimbali na kwenye Bajeti ya Mwakani tunakwenda kujenga nyumba nyingi za Walimu pamoja na kuboresha Maslahi yenu." Amesemq Rais Samia.


Akizungumza na walimu hao, Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Mb) Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka kwenda kushirikiana na wazazi na viongozi kuhakikisha wanafunzi wanajiunga na Masomo ifikapo Januari 08, 2024 wakati wa kuanza kwa Muhula wa Masomo bila kuchelewa.


Amebainisha kuwa kumekua na ongezeko la Ufaulu kwa watahiniwa wa Darasa la Saba hadi 1.57% ukilinganisha na mwaka 2022 hadi kupelekea wanafunzi 1,092,984 waliofaulu Mitihani ya Darasa la Saba kuchaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza katika Shule mbalimbali za Sekondari nchini 2024 hivyo ni lazima waenzi hali hiyo isishuke bali ipande.


Halikadhalika, amewataka watendaji ngazi zote kwenye Halmashauri na Mikoa kuhakikisha ifikapo Disemba 31, 2023 miradi yote ya Elimu iwe imekamilika ili kuwapa mazingira bora ya wanafunzuli kusoma na kwa Mkurugenzi ambaye hatafanya hivyo basi hatosita kumsimamisha ili aondolewe kwenye madaraka yao.


Rais wa TAHOSSA ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Ilboru Sekondari Denis Otieno amesema humuiya hiyo imejidhatiti katika kusimamia ufundishaji na ujifunzaji shuleni kwa mujibu wa miongozo iliyopo, kuthibiti utoro wa walimu na wanafunzi ili kusaidia kupandisha ufaulu pamoja na kusimamia nidhamu na maadili ya walimu shuleni.


"Kikokotoo imumekua msamiati ambao wastaafu wengi umekua ukiwaumiza si tu baada ya kuondoka kazini bali hata wakati wakikaribia kuondoka na kwakweli Mhe. Mgeni Rasmi tunaomba ukatusaidie kufikisha ombi letu la kuona namna ya kutafuta ufumbuzi kwenye suala hili." Rais TAHOSSA.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI Mhe. Denis Londo ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa Kutekeleza kwa vitendo adhma ya kuboresha Elimu nchini kwa kujenga miundombinu na kuboresha mitaala na ajira za walimu na akawataka walimu kujituma.


"Walimu ni Jeshi kubwa, hapa Mwanza mpo salama kabisa na mtakapokuja wakati mwingine mtaikuta ipo mahala pengine, tunazidi kusonga mbele kwa maendeleo na kwakweli tuna bahati sana maana miradi Mikubwa ya kimkakati ya Maendeleo nchini inafanywa Mwanza." Amesema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA Amos Makalla.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa