Wakuu wa shule zote za Sekondari Mkoani Arusha wametakiwa kuhakikisha wanatokomeza daraja la zero katika matokeo ya kidato cha nne kuanzia mwaka huu 2021.
Maagizo hayo yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Iddi Hassan Kimanta alipokuwa akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Arusha.
" Haiingii akilini mzazi anachangishwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa alafu mtoto wake anaishia kupata daraja la zero kidato cha nne", alisema Kimanta.
Kwa mkuu wa shule yeyote ambae shule yake itatoa daraja la zero atachukuliwa hatua kali,ikiwemo kuhamishwa kituo cha kazi.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Sanduku la Barua: 3050 Arusha
Simu: 27 254 5608
Simu Nyingine: 027 254 4950
Barua Pepe: ras@arusha.go.tz
Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa