• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

BALOZI DKT. NCHIMBI : LOWASSA ALIKUWA NI MCHAPAKAZI

Posted on: February 17th, 2024


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Balozi Emmanuel John Nchimbi, amesema Edward Ngoyai Lowassa alikuwa ni mtu aliyependa kufanyakazi, alikuwa ni mchapakazi, aliyezitumika nafasi zote alizokuwa nazo kwa weledi mkubwa.


Amesema, licha ya kuwa watu wanaweza kupishana katika maelezo ya kumwelezea

katika mambo mbalimbali, lakini jambo moja ambalo haliwezi kubishaniwa ni jinsi alivyokuwa mchakapakazi wa kweli, katika nafasi zake zote alizowahi kuzitumikia na katika kuwatumikia Watanzania wote. 


Dkt. Balozi Nchimbi amesema kupitia uhodari wake wa kuchapa kazi katika kutimiza wajibu wake kwa nchi, Hayati Lowassa alikuwa kiongozi mwenye uthubutu na uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya kutafuta ufanisi na kupata matokeo chanya ya haraka kwa ajili ya maendeleo ya watu. 


Dkt. Balozi Nchimbi amesema hayo leo Ijumaa, Februari 16, 2024 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kufika kuwapatia pole wafiwa, kusaini kitabu cha maombolezo na kutoa heshima za mwisho, nyumbani kwa Hayati Lowassa, katika Kijiji cha Ngarash, wilayani Monduli Mkoa wa Arusha, akiongeza kuwa kutokana na sifa za kiuongozi alizokuwa nazo, kifo cha kiongozi huyo ni pigo kubwa kwa nchi.


“Lowassa alikuwa mchapakazi kweli kweli. Alikuwa mtu wa maamuzi magumu. Watu wanaweza wakapishana katika kila maelezo wanayotoa kuhusu Lowassa lakini hakuna hata mtu mmoja anayeweza kuwa na ujasiri wa kusema alikuwa mvivu, au alikuwa hapendi kufanya kazi au hakuwa na mapenzi na nchi yake, hakuna. Alikuwa mchapakazi wa hali ya juu. Hakupoteza muda hata mara moja kuacha kufanya kazi kwa ajili ya Watanzania.


“Alikuwa mzalendo, mnyenyekevu na aliyependa watu wote bila kuwabagua. Moja ya uamuzi mgumu unaoendelea kukumbukwa ni hatua ya kiongozi huyo aliyoichukua ya kujiuzulu uwaziri mkuu mwaka 2008,” amesema Dkt. Nchimbi. 


Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesema taarifa za msiba huo wa Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa, ilikuwa ni mojawapo ya habari mbaya kwake kuwahi kuzipata. 


“Nimepoteza rafiki, kaka na mlezi. Lakini pia nimeona jinsi ambavyo chama changu kimepoteza mtu. Nimeona pia jinsi ambavyo nchi yetu imepoteza mtu. Nimeona jinsi ambavyo vyama vingine vilivyokuwa karibu naye vimepoteza mtu muhimu kwao. Pigo hili nililihisi binafsi na niliona ambavyo linaathiri nchi yetu.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa