• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA LONGIDO YATOA MAFUNZO YA KUBORESHA UANDIKISHAJI KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Posted on: December 5th, 2024

Katika hatua muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Longido imeandaa mafunzo ya siku mbili kwa wasimamizi wa uandikishaji wa ngazi ya kata. Mafunzo hayo, yamefanyika leo tarehe 4 na kumalizika  5 Desemba 2024 katika ukumbi wa Halmashauri, yalilenga kuimarisha mchakato wa uandikishaji wa wapiga kura wapya, kuboresha taarifa zilizopo, na kufuta majina ya wale waliopoteza sifa za kupiga kura.



Mafunzo hayo yaliwaleta pamoja maafisa wa kata kutoka kata zote 18 za Longido. Wakizungumza katika uzinduzi wa mafunzo hayo, viongozi wa uchaguzi waliweka wazi umuhimu wa zoezi hilo kwa mustakabali wa demokrasia na uwakilishi wa wananchi.



Akifungua mafunzo hayo, Msimamizi wa Uandikishaji wa Jimbo, Bw. Nevilling Lymo, aliwahimiza washiriki kuwa makini na weledi. “Zoezi hili si tu jukumu la kawaida; ni dhamana kubwa kwa taifa. Tunatarajia mtumie maarifa haya kuandikisha kila mwenye sifa, kuboresha taarifa sahihi, na kuhakikisha wale wasiostahili hawabaki kwenye daftari,” alisema.



Aliongeza kuwa ushirikiano baina ya wasimamizi wa kata na wasaidizi wao ni muhimu katika kufanikisha uandikishaji wa wapiga kura wenye sifa ili kuhakikisha usawa na haki katika uchaguzi ujao.



Afisa Uchaguzi wa Wilaya, Bw. Manase Msechu, naye aliwataka washiriki kuwa na utulivu na makini katika kufuatilia kila somo. “Hili ni zoezi nyeti linalohitaji umakini mkubwa. Kuboresha daftari kunatoa fursa kwa kila raia mwenye sifa kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi. Hakikisheni kila taarifa mnaijadili kwa kina na kwa usahihi,” alisisitiza.



Washiriki wa mafunzo hayo walionekana kufurahia mafunzo hayo, wakieleza kuwa yamewapa mwongozo bora wa namna ya kusimamia mchakato wa uandikishaji kwa ufanisi. Mafunzo hayo yameacha matumaini makubwa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2025 utakuwa wa haki na unaoaminika kwa pande zote.



Zoezi hili linachukuliwa kama hatua muhimu ya kuimarisha demokrasia na kuwapa wananchi wa Longido fursa ya kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya msingi ya kupiga kura.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa