• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI ZATAKIWA KUFIKIA 30% YA UWANDIKISHA BIMA YA AFYA

Posted on: August 3rd, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bwana Richard Kwitega ameziagiza halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kuhakikisha zinafikia malengo ya asilimia 30 ya uwandikishaji wa bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha tathimini ya mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa kwa nusu mwaka Mkoani Arusha.

Amesema malengo ya Kitaifa ni kuhakikisha asilimia 30 ya kaya zinafikiwa na huduma hiyo, hivyo hata Mkoa wa Arusha unatakiwa kuhakikihsa malengo hayo yanafikiwa kwa ukamilifu.

Aidha, amewataka waratibu wa mfuko wa bima ya afya kuhakikisha wanawafuatilia kwa ukaribu  wanachama wanaopata huduma hiyo katika vituo vya kutoa huduma ili kubainisha changamoto zinazojitokeza na kuzitatua kwa wakati.

Pia, amewataka wakurugezni wa halmashauri zote kuhakikisha vifaa vya uwandikishaji vinapatikana kwa haraka zaidi ili kuongeza kasi ya uwandikishaji.

Kwitega amesema bima ya afya iliyoboreshwa umelenga zaidi kutoa huduma za afya kwa wananchi hasa walioko kwenye mfumo wa ajira zisizo rasmi, ili kuwarahisishia kupata huduma za afya kwa urahisi.

Mratibu wa bima ya afya iliyoboreshwa bwana Denis Mgiye amesema, bima ya afya iliyoboreshwa ilianza rasmi Julai 1, 2019 hadi kufikia Julai 1, 2020 idadi ya kaya 7,557 zimeshajiunga na bima ukilinganisha na kaya 3,055 za mwaka 2019.

Amesema idadi hiyo imepelekea ongezeko la uwandikishaji kufikia asilimia 2 kimkoa na kushika nafasi ya 9 Kitaifa ukilinganisha na nafasi ya 23 kwa mwaka 2019.

Amesisitiza kuwa mpaka sasa wanufaika wa bima hiyo ya afya iliyoboreshwa kwa Mkoa wa Arusha ni watu 36,785 na Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ikiwa imesaidia kulipia kaya 1,300 zilizopo katika eneo la hifadhi hiyo.

Denis amesisitiza kuwa, mpaka sasa kiasi cha fedha shilingi milioni 91 kimeshapelekwa kwenye vituo vya kutolewa huduma vya Mkoa wa Arusha.

Amesema changamoto kubwa ni baadhi ya maafisa uwandikishaji kutopeleka fedha beki na hivyo kusababisha ucheleweshwaji wa utoaji huduma kwa wanachama.

Pia,ukosefu wa vifaa vya uwandikishaji kwasababu ya baadhi ya halmashauri kutolipa madeni kwa wakati.

Amesema mpaka sasa Mkoa umeweka mikakati mbalimbali ikiwemo, kila Kijiji kuandikisha kaya zisizopungua 31 kwa mwezi,kuhakikisha halmashauri zinalipa madeni ya kununua vifaa vya uwandikishaji na kuendelea kuhamasisha jamii kujiunga na bima ya afya.

Kikao hicho cha tathimini kilikuwa na lengo la kubaini hali halisi ya mwenendo wa huduma hiyo ya bima ya afya iliyoboreshwa tangu ilipoanzishwa mnamo Julai 2019 na mpaka sasa ikiwa imefikisha mwaka mmoja.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa