• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HEDHI SALAMA NI SWALA MTAMBUKA-DC KAGANDA

Posted on: August 10th, 2023

"Nendeni mkafanyie kazi mapendekezo yatakayotolewa kutokana na tafiti ya Oikos na E-MAC ili kuboresha zaidi mfumo mzima wa hedhi salama".

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Emmanuela Kaganda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa Mkoa katika kufanya tathimini ya mradi wa utafiti wa soko la taulo za Kike.

Amesema tafiti hiyo itasaidia katika kuboresha mazingira ya hedhi salama kwa wasichana na wakinamama.

Mhe.Kaganda amesisitiza zaidi kuwa hedha salama ni agenda ya Kitaifa na mtambuka kwani inahusu jinsia zote.

Hali kadhalika amesema, Serikali katika jitihada zake zakuhakikisha inaweka mazingira salama katika mfumo mzima wa hedhi salama kwa kuboresha miundombinu katika mashule.

Pia amesema katika juhudi hizo bado kuna changamoto ya gharama za vifaa  takribani 60% ya wasichana hawawezi kumudu gharama na hii inatokana na tafiti iliyofanywa na NIMRI 2021.

Vilevile 28% ya wasichana hawana elimu yakutosha juu ya matumizi sahihi ya vifaa hivyo.

Amesema kuna umuhimu mkubwa wa kutazama upya mnyororo wa thamani wa vifaa vya hedhi salama ili viweze kupatikana kwa urahisi.

Amesisitiza zaidi utumiaji wa mifumo ya kijamii katika kutoa elimu kwenye jamii ili kurahisisha zoezi nzima la utoaji elimu.

Nae, Afisa Afya na Mazingira kutoka Wizara ya afya Mariam Mashingo amesema juhudi zinazofanywa na Wizara hiyo nikuhakikisha jamii inavunja ukimya kwa wanaume kushirikishwa katika hedhi salama.

Pia, kuhakikisha wasichana na wanawake wanatumia bidhaa salama na zinazopatikana kwa urahisi kwasababu inagusa maswala mazima ya uzazi na afya kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa OIKOS Mary Birdi amesema shirika hilo likisaidiana na E-MAC wamefanya tafiti juu ya hedhi salama nakubaini kuwa wazazi wengi hawazungumzi na watoto wao pindi wanapofikia umri wa kupata hedhi.

Vile vile Upatikanaji wa vifaa vya hedhi bado nichangamoto hususani maeneo ya vijijini, hata pia gharama bado ipo juu kwa watumiaji wengi hawawezi kumudu.

Amesema utafiti wao uliangalia zaidi soko la vifaa lipoje kuanzia utengenezaji hadi kumfikia mtumiaji, kutambua wadau wanashughulika na hedhi salama na pia namna watakavyoweza kutekeleza zoezi zima la hedhi salama.

Mradi wa  utafiti wa soko la taulo za kike Tanzania Vijijini ulianza Januari 2023 katika shule za vijijini kwa Wilaya ya Karatu na Longido Mkoani Arusha.




Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa