• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YAKAGUA MRADI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI LAKE EYASI.

Posted on: March 9th, 2024


Na. Elinipa Lupembe 


Wajumbe wa Kamati ya Siasa mkoa wa Arusha, wametembelea na kukagua mradi wa shule mpya ya Sekondari Lake Eyasi, kijiji cha Laghangareri kata ya Mang'ola, wilaya ya Karatu na kujionea hali ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025.


Wajumbe wa kamati hiyo wamepongeza kazi nzuri inayofanywa na watalamu, viongozi na wananchi wa kijiji na kata, kwa ushirikiano wao katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuhakikisha ujenzi wa shule hiyo mpya umekamilika na tayari wanafunzi 124 wamekwishaanza masomo shuleni hapo, kuanzia mwezi Januari 2024.


Hata hivyo, licha ya kuwa mradi huo, umekamilika Mwenyekiti wa CCM mkoa, Loy Thomas Ole Sabaya, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Karatu, kufanyika kwa ukaguzi wa fedha zilizotumika kutekeleza mradi huo, kwa kuwa yupo mzabuni aliyetoa huduma ya mchanga na mawe bado anadai pesa za vifaa hivyo vya ujenzi.


Aidha, ameweka wazi kuwa licha ya changamoto hizo, bado Serikali ya Awamu ya sita inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha miundombinu ya kutolea huduma za kijamii, inajengwa maeneo yote nchini na kusogeza huduma karibu na wananchi hususani wananchi waishio maeneo ya vijijini.


"Wananchi wa Mang'ola tunakila sababu ya kuunga mkono juhudi za Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuhakiksiha wananchi wanapata huduma karibu na maeneo yao, tunaona zahanati, vituo vya afya zimejengwa, shule, barabara, huduma za umeme zinasambaa vijijini sasa, tuendelee kufanya kazi kwa bidii". Amesema Sabaya.


Shule hiyo ya Sekondari Lake Eyasi, imesajiliwa kwa namba S.6264, imejengwa na Serikali kwa gharama ya shilingi milioni 584.2 kupitia mradi wa kuboresha miundombinu ya shule za sekodnari nchini (SEQUIP)


Kiasi hicho cha fedha, kimejumuisha ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa, jengo la Utawala, Mabara za Masomo ya Sayanzi ya Fizikia, Baiolojia na Kemia, Maktaba, chumba cha TEHAMA, pamoja na vyoo vya wanafunzi. 


Awali, wananchi wa Mang'ola wameishukuru serikali ya Awamu ya sita kwa kujenga shule hiyo, ambayo imekidhi haja na matakwa yao, kutokana na watoto wao kuteseka kutembea umbali mrefu kufuata shule za sekondari, uliosababisha watoto utoro na baadhi ya watoto kuacha shule kutoakana sababu mbalimbali ikiwemo mimba za utoto kwa wasichana.


"Tunamshukuru sana Mama Samia, ujenzi wa shule hii, utawawezesha watoto kusoma jirani na nyumbani, jambo ambalo litapunguza utoro na mimba za utotoni, lakini tunategemea watoto wetu kusoma na kupata watalamu watakao litumikia Taifa letu baadaye" Wamesema wananchi wa kijiji hicho cha Laghangareri


#arushafursalukuki 




                        
                       
                        </div>
                        <!-- /.right-sidebar-content -->
                        <!--/END RIGHT SIDEBAR CONTENTE SECTION-->
                    </div>



<div class=

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa