• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MIMBA KWA WANAFUNZI ZA KITHIRI

Posted on: July 13th, 2018

Viongozi wa Kata wa halmashauri zote za mkoa wa Arusha watakiwa kutafuta suluhu ya tatizo la mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Akitoa maagizo hayo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Arusha,mkuu wa wilaya ya Karatu Theresia Mahongo katika kuhadhimisha siku ya kilele cha wiki ya elimu Mkoani Arusha.

Amesema changamoto kubwa iliyopo katika sekta ya elimu Mkoani Arusha ni mimba kwa wanafunzi hasa wa Sekondari,ambapo kwa mwaka 2017 wanafunzi 237 waligundulika kuwa na ujauzito ikiwa wanafunzi 50 ni wa shule za Msingi na 187 ni wa Sekondari.

Aidha,kuanzia Januari hadi Aprili 2018 jumla ya wanafunzi 97 waligundulika kuwa na ujauzito ambapo wanafunzi 17 niwa shule za Msingi na 80 wa Sekondari.

“Bado tatizo la ujauzito kwa wanafunzi wa kike ni changamoto kubwa hasa wa sekondari,wazazi bado mna jukumu kubwa hasa la kuhakikisha mnasimamia maadili ya watoto wenu na pia kuchangia fedha za chakula mashuleni ilikupunguza vishawishi kwa wanafunzi hawa”.

Katibu Tawala msaidizi upande wa elimu bwana Gift Kyando,amesema changamoto nyingine iliyopo katika sekta ya elimu Mkoani Arusha ni baadhi ya watoto kutojua kusoma,kuhesabu na kuandika (KKK), kwa sababu watoto hao hawapatiwi elimu ya awali kwanza kabla ya kujiunga na elimu ya msingi.

Amesema mbali na changamoto hizo,elimu bure kwa Mkoa wa Arusha imesaidia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa idadi ya uwandikishaji wa watoto darasa la kwanza.

Akisisitiza zaidi anasema mradi wa mpango wa kusaidia kusoma,kuandika na kuhesabu (LANES) umeweza kusaidia sekta ya elimu kwa kiasi kikubwa kwani mradi umeweza kuongeza Vitabu,Vifaa vya kufundishia na Vyombo vya usafiri,ambapo kila halmashauri itapatiwa kopyuta 3 za kusaidia utunzaji wa taarifa mbalimbali za wanafunzi.

Juhudi kubwa inaitajika katika kutoa kipaombele kwa watoto wenye ulemavu, kwani Mkoa unajumla ya watoto wenye ulemavu 614 ambao wanaitaji kuwa na madarasa maalumu lakini pia bado kuna baadhi ya wazazi wanawaficha watoto hao manyumbani.

Bwana John Isiriri ni mmoja wa wazazi waliohudhuria kilele cha wiki ya elimu,amesema ni kweli kuna tatizo kwa watoto wenye ulemavu kwa kutopewa kipaombale tokea katika ngazi ya familia zao na hivyo kupelekea wengi wao kukosa elimu.

Pia amesema tatizo la ujauzito kwa watoto wa kike bado ni changamoto kwa watoto wao hasa wa sekondari, lakini wazazi sasa wanatakiwa kusimamia maadili ya watoto wao na pia kuchangia chakula mashuleni ili kupunguza vishawishi kwa watoto wa kike.

Maadhimisho ya kilele cha wiki ya elimu hufanyika kila mwaka na mwaka huu 2018 kimkoa yamefanyika katika wilaya ya Karatu kwa lengo la kuhamasisha utoaji wa elimu bora kwa shule za mkoa wa Arusha.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa