• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA ARUSHA NI TEGEMEO KWA MZUNGUKO WA FEDHA ZA KIGENI.

Posted on: February 20th, 2024

Na Elinipa Lupembe 


Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa mikoa nchini inayotegemewa katika suala zima la mzunguko wa fedha za kigeni, fedha ambazo zinatokana na shughuli za Utalii pamoja na biashara ya nchi jirani ya Kenya kupitia Mpaka wa Namanga.


Hayo yamebainishwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, wakati wa mazungmzo mafupi yaliyofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kilichowakutanisha Bodi ya Wakurugenzi wa BoT na Menejiment ya mkoa wa Arusha.


Gavana Tutuba amesema kuwa, kutokana na onhezeko la watalii mkoani Arusha, mkoa huo umekuwa ni sehemu inayotegemewa katika upatikanaji wa fedha za kigeni kutokana na wageni hao, kutumia fedha hizo kwa matumizi yao wawapo mkoani Arusha.


Amesema kuwa, BoT imeendelea kuboresha na kurahisisha upatikanaji wa huduma za ubadilsihaji wa fedha nchini, huku mkoa wa Arusha ikiwa ni sehemu pekee ya kipaumbele kutoakana na mahitaji yanayotokana na idadi kubwa ya watalii wanaoingia na kutoka kila siku.


Aidha, Tutuba amempongeza Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassani kupitia Filamu ya 'Royal Tour', ambayo matunda yake yameanza kuonekana wazi hususani kwa wakazi wa mkoa wa Arusha.


"Tunatambua Arusha, imekuwa ni kitovu cha Utalii, ikiwemo utalii wa mikutano ya kimataifa na kitaifa, mikutano ambayo licha ya kuongeza mzunguko wa fedha za kigeni, inasaidia kusaidia kurecover kwa uchumi lakini zaidi ni kichecheo cha ukuzaji wa uchumi wa taifa " Amesema Tutuba.

Hata hivyo, serikali imelegeza mashari ya mitaji na kugikia milioni 5 kwa wazawa na kuwataka wakazi wa Arusha kuchangamkia fursa  hiyo kwa kuwekeza mitaji kwenye biashara na kwa wenye hoteli za kuanzia nyota tatu kufungua maduka ya kubadilishia fedha ndani ya hoteli zao kwa kuzingatia sheria zilizopo.


Hata hivyo Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Missaile Albano Musa, licha ya kumkaribisha Arusha Gavana Tutuba na Bodi nzima ya wakurugenzi wa BoT, amemuhakikishia hali ya usalama na utulivu wa mkoa wa Arusha, unaovutia wageni wengu kuendelea kuwepo Arusha.


Ameipongeza BoT kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kusimamia uchumi wa Taifa kupitia usimamizi imara wa fedha, unaosaidia mkoa wa Arusha licha ya kuwa na wageni wengi kutoka ndani na nje ya nchi, hakujawahi kutokea changamoto ya ukosekanaji wa fedha za kubadilisha.


Amebainisha kuwa, kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watalii nchini na kufanya shughuli nyingi za kitalii kufanyika mkoani Arusha, wananchi wa mko huo, wameendelea kunufaika na matunda ya filamu ya 'Royal Tour' ambayo imeongeza pato la mtu mmoja mmoja, familia, mkoa na Taifa pia.


Awali Gavana Tutuba yuko mkoani Arusha kwa shughuli za kikazi akiambatana na Bodi ya Wakurugenzi wa BoT ambao wanategemea kupatiwa mafunzo ya uendeshaji wa Bodi hiyo.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa