• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

NITAFANYA KAZI KWA KARIBU SANA NA WAFANYABIASHARA-KIMANTA

Posted on: July 2nd, 2020

“Nitasimamia mazingira ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha yawe mazuri na rafiki kwenu kwa kuyatambua na ikiwezekana kutatua changamoto zenu”.

Yamesemwa hayo na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Idd Kimanta alipokuwa akizungumza na viongozi wa vyama mbalimbali vya wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha,jijini Arusha.

Amewataka wafanyabiashara kutumia ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa karibu sana kwa kuleta changamoto zao kwa uhuru kupitia idara ya Uchumi na Uzalishaji mali.

Aidha, amewashauri wafanyabaishara kuwa na mazoea ya kuchukua mikopo katika mabenki ili iwasaidie kukuza biashara zao kwa kasi sana na kuongeza tija.

Pia, amewasisitiza kuendelea kulipa kodi hata kama kuna changamoto zimejitokeza hasa katika kipindi hiki ambapo dunia ilikubwa na ugonjwa wa Corona, amesema kodi zinasaidia sana kuleta maendeleo yote ambayo yanaonekana kwa sasa katika nchi.

Vile vile amewataka wafanyabiashara wadogo hali maarufu kama (wamachinga) kuzingatia usafi wa mazingira  pindi wanapofanya biashara zao kwenye maeneo yao, hii itasaidia kuliweka jiji la Arusha katika mazingira safi.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara wote mwenyekiti wa chama cha waendeshaji wa shughuli za watalii (TATO) bwana Wilbrod Chambulo, amesema wao wataendelea kushirikiana na serikali kwa karibu zaidi.

Amemuomba Meneja wa Mamlaka ya MapatoTanzania (TRA) kutenga dirisha maalumu la kuhudumia wafanyakazi waliopunguzwa kazi kwenye makampuni mbalimbali ya Utalii kutokana na janga la Korona ili kuwapunguzia adha ya kukaa katika foleni.

Chambulo amesema, mabenki mengi yamekuwa msaada mkubwa sana kwa wafanyabiashara kwa kutoa mikopo na amewashauri wafanyabiashara wenzake kutumia mabenki kuweka fedha zao badala ya kukaa nazo nyumbani.

Akijibu hoja hizo Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania bwana John Mwigulwa amesema, tayari TRA wameandaa dirisha maalumu la kusikiliza mahitaji mbalimbali ya wateja wao hususani wanaotoka katika sekta ya Utalii.

Aidha , amewataka wafanyabiashara kuwa waaminifu katika kipindi hiki ambacho dunia imekubwa na ugonjwa wa Corona kwani wapo baadhi yao wanatoa taarifa za kufunga biashara zao lakini mifumo ya TRA inaonesha bado wanafanyabiashara.

Mheshimiwa Kimanta, amejitambulisha rasmi katika jumuiya ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha na kuwaomba kufanya kazi kwa ushirkiano mkubwa na serikali yao ili kuleta maendeleo ya Mkoa na nchi kwa ujumla.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa