• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELA AWASIHI WANANCHI KUTEMBELEA MAONYESHO YA WIKI YA HUDUMA ZA KIFEDHA YANAYOENDELEA MKOANI ARUSHA.

Posted on: November 21st, 2023


Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella, ametembelea Mabanda ya Maonesho ya tatu ya Wiki ya Huduma za Kifedha, yanayoendelea kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abed Jijini,  Arusha, na kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi, kutembelea maonesho hayo muhimu ili kupata ufahamu wa huduma sahihi za kifedha.

Mhe. Mongella amesema kuwa maonesho hayo ni muhimu kwa Umma na kuwataka wakazi wa Arusha na mikoa ya jirani, kufika kwenye mabanda hayo ili kupata elimu ya huduma sahihi na rasmi za kifedha pamoja na kuzitambua taasisi zinazotoa huduma za kifedha ili kuepukana na taasisi za kitapeli.

Ameweka wazi, kuwa kumekuwa na changamoto ya uelewa mdogo wa wananchi, juu ya huduma za kifedha na kusababisha baadhi yao kutapeliwa, kwa kujiingiza kwenye mikopo inayoumiza, na baadaye kuingia kwenye migogoro ya kisheria bila kutegemea, na kusisitiza kuwa maonesho hayo ndio sehemu sahihi ya kupata uelewa na kufanya maamuzi ya kuchagua huduma sahihi na inayofaa.

"Niwasihi wananchi wote, kufika kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abeid, licha ya kupata elimu juu ya huduma za kifedha, zaidi ni fursa ya kuzitambua taasisi rasmi za kifedha ili kufanya maamuzi sahihi wakati wa kuchagua huduma ipi ya kuitumia" Amebainisha Mhe. Mongella.

Naye Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Janeth Hiza, amefafanua kuwa, maonesho hayo yana lengo la kutoa elimu kwa Umma, juu ya Huduma za kifedha pamoja na kuwajengea uwezo wa kuelewa juu ya matumizi sahihi ya huduma rasmi za kifedha, zitakazosaidia katika utunzaji wa fedha zao, matumizi ye fedha, kuweka na kukopa, ili kukuza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.

Inafahamika kuwa, Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ni utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa Mwaka 2020/21 - 2029/30, ambao Elimu kwa Umma ni moja ya maeneo ya kipaumbele katika utekelezaji wake.

Aidha, Maonesho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Kifedha Mwaka 2023 yenye Kauli Mbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi, yameratibiwa na Wizara ya Fedha kwa ushirikiano wa wadau wengine wa fedha wakiwemo benki kuu ya Tanzania huku jumla ya Benki 35 zikishiriki na kutoa fursa kwa wananchi kuzifahamu benki hizo na huduma zake.








Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa