• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AWAPA SIRI ZA MAFANIKIO WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA SHULE YA SEKONDARI MLIMANI MURIET – JIJI LA ARUSHA

Posted on: January 8th, 2024

Na. Daniel Gitaro

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella amepata wasaa wa kuzungumza na wanafunzi waliojiunga na kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Mlimani Muriet muhula wa masomo 2024 wakati alipotembelea shule hiyo kukagua maendeleo ya mapokezi ya wanafunzi waliopangiwa shuleni hapo.

Mhe. Mongella amewaasa wanafunzi hao kwa mambo kadha wa kadha ikiwemo kuwa na nidhamu, kufanya kazi kwa bidii huku wakimwamini Mungu katika masomo yao sambamba na kuwa na malengo.

Aidha amewataka viongozi maafisa Elimu pamoja na Watendaji wa Vijiji na Kata kuendelea kuwahamasisha wazazi kuwaandikisha watoto waliofika umri wa kuanza shule kwa kuwa Serikali imeshafanya sehemu yake ya kuandaa mazingira bora kwa ajili ya watoto wa Kitanzania kupata Elimu.

“Serikali imekwisha tekeleza majukumu yake ya kuleta fedha zilizotekeleza ujenzi wa miundombinu rafiki kwaajilli ya watoto  kupata elimu iliyo bora, viongozi sasa ni wajibu wetu kuhamasisha wazazi kuwaandikisha watoto waliofika umri wa kuanza shule.” Amesema Mhe. Mongella.

Hata hivyo, ametoa rai kwa viongozi wa Jiji la Arusha kuongeza umakini katika kusimamia utekelezaji wa miradi katika viwango vinavyostahili kwa kuwa Serikali inatoa fedha nyingi za kutekeleza miradi hiyo.

Aidha, wanafunzi hao, licha ya kumshukuru Mkuu huyo wa Mkoa kwa kuwatembelea na kuwatia moyo katika safari hiyo mpya ya masomo waliyoianza, wameishukuru Serikali kwa kuwaandalia mazingira bora ya ujifunzaji yatakayowawezesha kutimiza ndoto zao.

“Tunaishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kazi kubwa na kutujengea shule nzuri yenye walimu wazuri, tunaahidi kusoma kwa bidii na kufaulu.” Amesema Noel Emmanuel, Mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Mlimani Muriet.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Beatrice Gregori Tarimo ameahidi kuendelea kusimamia taaluma kwenye shule hiyo sambamba na miradi itakayoendelea kutekelezwa shuleni hapo ili kufikia malengo ya Serikali.

Awali, shule hiyo ilipangiwa kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 200 na hadi sasa wanafunzi walioripoti ni 177, wavulana ni 84 huku wasichana wakiwa ni 93.














Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa