• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YATIMIZA AHADI, YAANZA KUTOA VITAMBULISHO VYA NIDA, KWA WALIOJIANDIKISHA ARUSHA....

Posted on: December 1st, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, imetimzia ahadi yake wka wananchi, kwa kuanza kutoa vitambulisho vya Taifa, maarufu kama NIDA, kwa wananchi waliojianzikiwasha nchini, mkoa wa Arusha ukiwa miongoni mwao, zoezi ambalo lilikwama kwa zaidi ya miaka minne sasa.


Akizungumza wakati wa akizindua zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya NIDA kimkoa, wilayani Karatu, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K.Mongella, amesema kuwa, Serikali imekamilisha ahadi yake kwa wananchi  waliojiandikisha kwa kuanza kuwagawia vitambulisho vyao vya taifa huku akiwahakikishia wakazi wa mkoa huo kuwa, kila mwananchi mwenye sifa atapata kitambulisho cha Taifa.


Amesema kuwa, takribani watu 931,221, waliojiandikisha mkoani hapo, watapata vitambulisho, na tayari vitambulisho 880,000 vimeshafika kwenye ofisi za NIDA wilaya zote za mkoa huo, tayari kugawanywa kwa wananchi.


Leo nimekabidhi vitambulisho 99,132 kwa Maafisa Watendaji wa kata za Wilaya ya Karatu, ili wakawakabidhi Watendaji wa vijiji na viwafikie wananchi kwenye maeneo yao.


Aidha amewaagiza Maafisa Watendaji, kuhakikisha vitambulisho hivyo vinagawiwa kwa walengwa ndani ya siku 14, na kwa waliofariki dunia vitambulisho visitolewe, bali virejeshwe Ofisi za NIDA za wilaya.


"Rai yangu kwa Watendaji wote, kila kitambulisho akabidhiwe mhusika mwenyewe, kusitokee ubabaishaji wowote, kwa mtu aliyefariki rudisheni taarifa zake NIDA, asikabidhiwe kitambulisho mtu asiyehusika"Ameweka wazi


Amesisitiza wananchi wenye sifa, kuona umuhimu wa kuwa  na kitambulisho cha Taifa, kwa kuwa mwelekeo wa Serikali sasa, ni kuingiza taarifa za kila mtanzania kwenye mfumo wa kidijitali, ambao utarahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa kila mtanzania.


Hata hivyo wananchi wa Karatu wameishukuru Serikali, kupitia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa vitambulisho vyao, ambavyo wamekuwa wakivisubiri kwa muda mrefu huku wakipata usumbufu mkubwa, ikiwemo kukosa baadhi ya huduma zilizohitaji kuwa na kitambulisho hicho.


Bupe Alfred Mwankusye, mkazi na mjasiriamali wa Karatu mjini, ameweka wazi kuwa, licha ya kuishukuru Serikali kwa kuwakabidhi vitambulisho vyao na kuongeza kuwa, kutokuwa na vitambukisho vya NIDA, walikwama kwenye masuala ya mikopo kutoka Taasisi za fedha ambazo zililazimu kuwa na kitambulisho hicho


"Tunamshukuru mama Samia kwa kutupa vitambulisho, wananchi tuliteseka, hasa wajasiriamali tulipohitaji kuchukua mikopo ya kuendeleza biashara, kwa sasa mambo yetu yatakwenda kama tunavyopanga" Amesema Mwajabu Khasim,


"Tulipia changamoto nyingi, kuna wakati  nilimpeleka mtoto shule, nikapata usumbufu sana kwa kutokuwa na kitambulisho cha NIDA kwa sasa tunasema Kazi iendelee". Martina Philipo.


Ikumbukwe kuwa, ugawaji wa vitambulisho vya Taifa kwa watanzania, ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020 - 2025


#ArushaFursaLukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa