• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SHAMBA LENYE UKUBWA WA EKARI 43.5 LAKABIDHIWA KWA SERIKALI.

Posted on: April 30th, 2022

Shamba lenye ukubwa wa ekari 43.5 lililokiwa likimilikiwa na Kampuni ya Tanzania Plantations limekabidhiwa rasmi kwa Serikali kwa ajili ya kuliendeleza zaidi.

Makabidhiano ya shamba hilo yamefanyika katika Kijiji cha Bwawani kata ya Bwawani ndani ya Halmashauri ya Arusha.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo Waziri wa ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula amesema, makabidhiano hayo yamefikiwa baada ya mwekezaji huyo kutoka Kampuni ya Tanzania Plantations kukiuka masharti ya uwekezaji mnamo mwaka 1999.

Waziri Mabula amesema, maamuzi hayo ya kulirudisha shamba hilo chini ya Serikali ni kwa manufaa ya Serikali na wananchi hasa wa eneo hilo.

Amesisitiza zaidi kwa wananchi wa Kijiji cha Bwawani kuwa na subira ya kusubiri Serikali inaweka mpango mzuri wa matumizi ya ardhi hiyo,hivyo wasifanye shughuli zozote katika shamba hilo hadi utaratibu huo utakapokamilika.

Mhe.Mabula amesema, mpango wa matumizi bora ya shamba hilo utafanyika ndani ya miezi 3 tu na wakazi wa eneo hilo ndio watapewa kipaombele.

Aidha amesema hatua za mpango wa matumizi ya shamba hilo utakuwa shirikishi na wananchi wa eneo hilo watashirikishwa kwa ukaribu zaidi.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongella amewataka wananchi wa Kijiji hicho kutogeuza shamba hilo kama shamba la Bibi kwa kutaka kufaidi zaidi.

Pia amewataka viongozi wa Kijiji na Kata kutopata ushawishi na kuleta watu kutoka nje ya Kijiji hicho ili nao waweze kunufaika na shamba hilo.

Aidha, amemuakikishia Waziri kuwa zoezi la kuandaa mpango wa matumizi ya shamba hilo utafanyika kwa haraka na kwa muda uliopangwa na wananchi watahusika kwa kiwango kikubwa.

Nae, Katibu Mkuu Wizara ya ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt. Allan Kijazi amesema Kampuni ya Tanzania Plantations imelipwa jumla ya Bilioni 5.7 na Serikali baada ya Kampuni hiyo kufungua mashauri dhidi ya Serikali kwa kuvunja mkataba wa umiliki wakati Kampuni hiyo ilishawekeza mali nyingi kama Nyumba na mashine za kutengeneza katani.

Amesema mnamo mwaka 2015 Kampuni hiyo iliamua kuondoa shauri hilo mahakamani na makubalino ya malipo ya fedha hizo yakafanyika nje ya Mahakama na Serikali haidaiwi na Kampuni hiyo.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Plantations Bwana  Pradip Lodhia ameishukuru Serikali kwa kumaliza shauri hilo kwa amani na amefurahi  kukabidhi shamba hilo kwa Serikali.

Nae, Diwani wa Kata ya Bwawani Justine  Rengatia ameiomba Serikali itakapoamua kuwauzia shamba wananchi wa Kijiji hicho basi wapewe muda wa kulipa kwa awamu kutokana na hali ya uchumi wao kuwa duni.

Mgogoro wa shamba hilo umedumu zaidi ya miaka 20 na ulikuwa kati ya Serikali na aliyekuwa mmiliki wa shamba hilo kampuni ya Tanzania Plantations na umemalizwa mnamo mwaka 2022.





Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa