• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TRC YAANZA MCHAKATO UJENZI WA RELI YA KISASA YA SGR MKOANI ARUSHA

Posted on: March 25th, 2025

(Jumanne, Machi 25, 2025 – Arusha) Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Bw. Masanja Kadogosa, kuhusu mpango wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) itakayounganisha mikoa ya Kaskazini.



Katika mkutano huo uliofanyika ofisini kwake Jijini Arusha, Bw. Kadogosa alieleza kuwa serikali tayari imeanza taratibu za ujenzi wa reli hiyo, mradi unaotekelezwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kama sehemu ya maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Ujenzi huu unalenga kuboresha miundombinu ya usafirishaji na kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha na kanda nzima ya Kaskazini.



Akizungumza kuhusu manufaa ya mradi huo, Bw. Kadogosa alisema kuwa reli hiyo ya kisasa itakuwa chachu ya maendeleo kwa Arusha, hasa kwa sekta ya uchumi, biashara na madini. Alifafanua kuwa uwepo wa madini ya soda katika mkoa huo ni rasilimali muhimu, huku akibainisha kuwa machimbo ya madini hayo yana uwezo wa kudumu kwa zaidi ya miaka mia moja. Aidha, alieleza kuwa ujio wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga utahitaji mfumo madhubuti wa usafirishaji wa mafuta ghafi, na reli hii itakuwa njia mojawapo muhimu ya kusafirisha mafuta hayo hadi masoko ya kimataifa.



Kwa upande wake, Mhe. Makonda alimshukuru Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa unaofanyika katika Mkoa wa Arusha, akiahidi kuwa wakazi wa mkoa huo wataendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazoletwa na serikali ya awamu ya sita. Pia, alisisitiza kuwa Arusha imejipanga kuweka rekodi kwa idadi kubwa ya kura kwa Rais Samia katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu kama ishara ya shukrani kwa miradi inayotekelezwa, ikiwemo ukuzaji wa uchumi, uimarishaji wa sekta ya utalii na madini, na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara.



Katika hatua nyingine, Mhe. Makonda alibainisha kuwa Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wizara ya Madini umeanza maandalizi ya maonesho ya madini yatakayofanyika kila mwaka, hatua itakayosaidia katika kutangaza na kuendeleza sekta ya madini nchini.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa