• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUMIENI FURSA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI-RC SENDIGA

Posted on: August 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga amewataka waoneshaji na wananchi kutumia fursa zilizopo kwenye kilimo ,uvuvi na ufugaji ile ziweze kuleta tija kwani fursa zinafuatwa na hazimfuati mtu.

Amewataka wataalamu wa sekta hizo husika wakajipange kutoa elimu katika maeneo yao badala yakusubiri maonesho ya nanenane ili wakulima na wafugaji  wapate elimu hiyo.

Amesisitiza kuwa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi amewashauri wananchi watumie fursa ya kilimo cha umwagiliaji zaidi kwani maeneo yapo yakutosha katika Mikoa yote mitatu.

Serikali ya Dkt. Samia imeendelea kutenga fedha zaidi katika sekta ya kilimo  na kwa kanda ya Kaskazini zaidi ya  bilioni 47.6 zimetolewa ili kukuza Kilimo zaidi hasa kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji.

Mwaka wa fedha 2022/2023 serikali imepanga kuchimba visima takribani 150 kwa kila halmshauri ili kurahisha upatikanaji wa maji yatayorahisisha kilimo cha umwagiliaji.

Amezitaka Halmshauri zote kanda ya Kaskazini kutoa ushirikiano kwa tume ya uwagiliaji itakapoanza zoezi la kubainisha maeneo ya uchimbaji visima hivyo kwa kuwashirikisha wananchi.

Amewataka wafugaji kushirikiana na serikali katika kutumia teknolojia ya ufugaji wenye tija kwa kuwa na mifugo michache zaidi kutokana na upungufu wa maeneo ya malisho.

Kutunza mifugo michache ni rahisi zaidi kuliko mifugo mingi kwani gharama inakuwa chini na pia mfugaji atapunguza msongo wa mawazo.

Amewataka wakulima na wananchi kuona namna yakuongeza mnyororo wa thamani ili mazao yaweze kuleta tija zaidi.

Amezitaka Halmashuri kutunza fedha zinazotolewa kama ushuri unaotoka kwenye kilimo na uvuvi zirudi kwenye maeneo husika ili zikaleta mabadiliko zaidi kwenye maeneo hayo.

Akizungumza katika maonesho hayo Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella amesema maonesho hayo yataendelea kuboreshwa kila mwaka ili yaongeze tija zaidi kwa waoneshaji na wananchi.

Kwa upande wake,Mkuu wa wilaya ya Moshi Kisare Makori kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu amesema maonesha haya yanawapa fursa wakulima na wafugaji  wakuonesha mazao yao na pia kutoa elimu kwa wananchi.

Ameshauri  SIDO kufanya kazi kwa karibu na wafanyabiashara ili kuwapa elimu ya utengenezaji bora wa bidhaa itakayowawezesha kupata masoko yakutosha.

Pia, amewashauri Shirika la viwango Tanzania TBC kufanya kazi kwa karibu na wafanyabiashara hao ili waweze kupata vibari vya ubora kwa haraka.

Hata hivyo, amezitaka halmshauri kupitia kwa maafisa ugani kutoka nje ya ofisi zao ili kutoa elimu yakutosha kwa wakulima kwa lengo la kuzalisha mazao yenye ubora na yatayokubalika katika masoko mbalimbali.

Nae, Mwenyekiti kamati ya maandalizi ambae pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Missaile Musa amesema kwa maonesho ya mwaka 2023  jumla ya washiriki 220 kutoka Taasisi na Kampuni zimeshiriki katika maonesho hayo.

Maadhimisho ya siku ya wakulima na sherehe za nanenane Kanda ya Kaskazini yamefanyika katika viwanja vya Themi Njiro Mkoani Arusha na yakiwa yamebeba kauli mbiu isemayo "Vijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula" na Mikoa iliyoshirikia ni Arusha, Manyara na Kilimanjaro.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa