• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUMIENI MAJINA YATAKAYO ACHA HISTORIA YA NCHI

Posted on: April 12th, 2022

Na.Mwandishi wetu, Arusha


Waziri wa Habari, mawasiliano na teknolojia ya habari, Mhe. Nape Nauye ametoa wito kwa Halmashauri zote nchini kutoa majina katika Mitaa na barabara ambayo yatakuwa na kumbukumbu ya historia ya nchi kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na   viongozi mbalimbali wa Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Arusha akiwa katika oparesheni maalumu ya kukagua zoezi nzima la anwani za makazi.

Majina hayo yatasaidia kutunza historia ya nchi kama kutumia majina ya viongozi mbalimbali au wabunifu.

Amesema kwa Mkoa wa Arusha anwani za makazi zitasaidia sana utalii kwani watalii wataweza kutumia mfumo huo kufika mahali wanapotaka kwa urahisi zaidi.

Mhe. Nape amesisitiza umuhimu wa kuwa na anwani za makazi ni urahisi wa kuhudumiwa,  kuwasiliana na hata kukutana kistaarabu.

Aidha, amewaomba viongozi wa dini kuhamasisha waumini wao walione kama nila kwao ili kuendelea kumuunga Mkono Rais wetu.

Pia, ameupongeza Mkoa wa Arusha kwa kuendelea kufanya vizuri zoezi hilo japokuwa mazingira ya Mkoa niya kusambaa lakini bado zoezi linakwenda vizuri.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amemwakikishia Waziri kuwa zoezi hilo litakamilika ifikapo Aprili 30,2022 kabla ya ile tarehe ya Kitaifa Mei 30.

Amesema Mkoa unaendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ili walichukulie zoezi hili kama la kwao.

Nae, Katibu Mkuu wa Wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Dkt. Jim Yonazi ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa kubuni kalakana inayosaidia kupunguza gharama za utengenezaji wa mabomba.

Amesema wizara yake itaendelea kutoa ushirikiano ili kuwezesha zoezi hilo kukamilika vizuri na kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe.Said Mtanda amesema Wilaya yake imeshatambua jumla ya nyumba 122,000 na zoezi zima limeshafikia asilimia 78.

Akitoa taarifa ya Mkoa, Katibu Tawala msaidizi Mipango na uratibu bwana Said Mabiye amesema zoezi la kuweka anwani za makazi lilizinduliwa rasmi mnamo Februari 12,2022 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Amesema zoezi hilo hadi sasa linatumia mfumo wa kijitali unaonesha kiwango cha uwekaji wa Anwani za makazi katika  Mkoa mzima.

Mhe. Nape amefanya Operasheni ya anwani za Makazi kwa siku moja Mkoani Arusha ambapo amefanya kikao na viongozi mbalimbali wa Mkoa na Jiji la Arusha na pia aliweza kagua uwekaji wa vibao katika Barabara na Mitaa na amekagua kalakana inayotengeneza mabomba ya vibao vya majina katika Jiji la Arusha.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa