• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

*TUTAENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WALIMU-MAJALIWA.*

Posted on: December 13th, 2024

_Asema Rais Dkt. Samia anatambua na kuthamini kazi kubwa wanayoifanya_



WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuendelea kutatua changamoto za walimu zikiwemo za malimbikizo ya madeni na upandishaji wa madaraja.



Amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua, anathamini na kuheshimu kazi kubwa inayofanywa na walimu wote nchini katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kukuza na kuiendeleza sekta ya elimu nchini.



Amesema hayo leo (Alhamisi, Desemba 12, 2024) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 19 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Jakaya Kikwete jijini Dodoma



“Kwa sasa suala la stahiki za walimu linaendelea kuzingatiwa na Serikali imeendelea kufanya jitihada kubwa za kuhakikisha inapadisha madaraja watumishi walimu waliokosa na wanaopaswa kupandishwa, Serikali imedhamiria kuondoa msamiati wa arears (malimbikizo ya mishahara).”



Amesema kuwa katika kipindi cha (mwaka 2021/2022 hadi mwaka 2023/2024), Serikali imepandisha madaraja ya walimu 227,383 na kuwabadilishia miundo walimu 20,436.“ Ofisi ya Rais-TAMISEMI hakikisheni kila anaepanda daraja analipwa stahiki zake kwa wakati.”



Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi cha 2021/22 hadi 2023/24, jumla ya shilingi trilioni 1.76 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya shule ikiwemo ukarabati na ujenzi mpya.



“Miundombinu hii imesaidia kwa kiasi kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shuleni.”



Akizungumzia kuhusu utekelezaji wa Sera ya Elimu bila Malipo, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali imeendelea kutoa shilingi bilioni 33.3 kwa mwezi kwa ajili ya shule zote za Msingi na Sekondari za Serikali nchini ikiwa ni za uendeshaji wa shule pamoja na posho za madaraka.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa