• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

VIJANA ZAIDI YA 1, 000 WAJITOKEZA KWENYE USAHILI WA UFADHILI WA MASOMO NCHINI INDIA

Posted on: March 26th, 2025

Mapema leo Machi 26, 2025 vijana zaidi ya 1000 wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa katika ofisi za mkoa kwa ajili ya usahili wa kuwania nafasi za ufadhili wa masomo nchini India kufuatia tangazo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, aliyesema kuwa serikali ya India imetoa ufadhili wa masomo kwa vijana 1,000 wa Arusha.



Akizungumza wakati wa ufunguzi wa usahili huo, Mhe. Makonda amebainisha kuwa ufadhili huo utahusisha programu na fani zaidi ya 250, ufadhili huo ukisimamiwa na Serikali ya India kupitia kwa Balozi wake nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey.



Mhe. Makonda ameeleza kuwa fursa hiyo imetokana na juhudi kubwa alizozifanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha uhusiano na mzuri na Mataifa Mengine ambazo zimepelekea nchi kama India kutoa fursa hizo kwa vijana wa Kitanzania.



"Hii ni fursa adhimu kwa vijana wa Arusha kupata elimu bora nje ya nchi, hususan nchini India, ambayo inajulikana kwa ubora wa elimu yake katika nyanja mbalimbali," amesema Mhe. Makonda.



Hata hivyo Mhe. Makonda ameendelea  kusisitiza umuhimu wa vijana kujitokeza na kutumia fursa hizi ili kuleta maendeleo binafsi na ya taifa kwa ujumla.



Katika hatua nyingine ya ushirikiano huo, Serikali ya India imetoa ufadhili kwa Wajasiriamali 50 wa Arusha kusomea kozi ya Upishi nchini India. Lengo ni kuwawezesha kujifunza mapishi ya vyakula vya Kihindi na tamaduni mbalimbali za taifa hilo, ili kuboresha huduma kwa watalii wa Kihindi wanaotembelea Tanzania.



Kwa upande wao, vijana waliojitokeza katika usahili huo wameelezea furaha yao kwa fursa hii adhimu, wakisema kuwa ni hatua kubwa kwao katika kufikia malengo yao ya kielimu na kimaendeleo.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa