• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WATANZANIA TUJIAMINI TUNAWEZA KUFANYA MAMBO MAKUBWA-RAIS MAGUFULI

Posted on: October 24th, 2020

Zaidi ya mabehewa 800 ya mizigo kununuliwa yakiwemo yenye majokofu ili kurahisisha usafirishaji wa maua na mbogamboga ndani na nje ya nchi.

Ahadi hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizundua rasmi usafiri wa treni kutoka Dar es Salaam hadi Arusha kupitia Tanga na Kilimanjaro, katika stesheni za Reli Jijini Arusha.

Amesema wakulima wakubwa wa maua na mbogamboga wapo katika Mkoa wa Arusha hivyo atawarahisishia wafanyabiashara hao katika kupata soko la ndani na nje kupitia reli hiyo.

Amesisitiza zaidi katika maboresho ya huduma za reli nchini, serikali yake itanunua vyichwa vya treni vipatavyo 36 na mabehewa 37 ya abiria.

Amewataka watanzania kujiamini kuwa wanaweza kufanya mambo makubwa ya maendeleo katika nchi yao,hivyo wailinde na kuitunza reli hiyo ili iweze kuwanufaisha vizazi hadi vizazi.

Rais Magufuli amesema treni hiyo inamanufaa makubwa katika kukuza uchumi wa nchi,kupunguza bei za usafarishaji wa abiria na mizigo na kuokoa muda wa usafirishaji.

Akisoma taarifa ya mradi wa ufufuaji wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Arusha Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Reli Tanzania bwana Masanja Kadogosa, amesema treni hiyo ilisimamisha huduma zake tokea mwaka 1986 na sasa serikali ya awamu ya tano imetumia bilioni 14 kurudisha huduma hiyo katika mikoa hiyo ya Kaskazini.

Kadogosa amesema, tokea huduma hiyo kurejeshwa takribani tani 2600 za mizigo zimeshasafirishwa ndani ya mwezi mmoja na abaria wapatao elfu 55 wameshatumia usafiri huo kutoka Dar es Salaam hadi Arusha.

Aidha, amesema usafiri huo wa treni umelenga kutoa huduma kwa wananchi wote hususani wananchi wa kawaida na wafanyabiashara wadogo, ndio maana na hata bei zake zinakidhi hali ya mtanzania.

Nae Theresia Mollel Mkazi wa Jiji la Arusha, amesema kurejeshwa kwa huduma hizo za treni kwa Mkoa wa Arusha kutawasaidia wao kama wakazi kupunguza gharama za usafiri kutoa Dar es Salaam hadi Arusha na pia itawasaidia kuokoa muda wa kusafiri barabarani.

Theresia ameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kurejesha huduma hiyo ya treni na maendeleo mengine yote yaliyofanywa na awamu hiyo.

Uzinduzi wa treni ya abiria na mizigo Kanda ya Kaskazini umefanywa rasmi baada ya huduma hiyo kuadimika zaidi ya miaka 30 na uzinduzi huo umeshihudiwa na viongozi mbalimbali wa serikali na dini.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa