• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKALLA: DKT. SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA AFYA MKOANI ARUSHA..

Posted on: September 9th, 2025

 _Amshukuru Mhe.Rais Dkt.Samia kwa kutoa Milioni 900 kuboresha miundombinu Hospitali ya Wilaya ya Meru_


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla @amosmakalla amemshukuru Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mapinduzi makubwa kwenye sekta ya afya Mkoani Arusha, huku Hospitali ya Wilaya ya Meru Wilayani Arumeru ikipokea shilingi Milioni 900 zilizotolewa kuboresha miundombinu ya huduma za afya hospitalini hapo.


CPA. Makalla ameyaeleza hayo leo Jumanne Septemba 09, 2025 alipotembelea na kukagua hali ya utoaji na uoatikanaji wa huduma kwenye majengo mapya manne ya Hospitali hiyo ikiwemo Jengo la wagonjwa wa nje, Jengo la Maabara, Jengo la Bohari ya dawa pamoja na jengo la kuchomea taka pamoja na jengo la wagonjwa wa dharura, majengo ambayo tayari yameanza kutoa huduma kwa wagonjwa, yakitajwa kupunguza muda wa utoaji wa huduma kwa mgonjwa kutoa saa nane hadi saa mbili.


"Faida za uwekezaji huu mkubwa ni pamoja na kupunguza masaa ya kuwahudumia wagonjwa kutoka saa nane mpaka saa mbili, uwepo wa vipimo 38 ambavyo vimepunguza rufaa za wagonjwa kwenda kwenye hospitali za rufaa kama vile KCMC na Mount Meru, haya ni mafanikio makubwa kwa serikali yetu, niwaombe watoa huduma wote kupitia uwekezaji na maboresho haya,  vitafsiriwe kwa ninyi kutoa huduma bora kwa wagonjwa, kuanzia mapokezi, lugha nzuri mpaka kwenye huduma za matibabu." Amesema CPA. Makalla.


Aidha, CPA Makalla, amesisitiza kuwa,  mapinduzi hayo makubwa kwenye sekta ya afya yameambatana na ongezeko kubwa la bajeti kwaajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba katika hospitali hiyo pamoja na ukarabati wa jengo la watoto njiti na watoto wachanga wenye kuhitaji uangalizi maalumu.


Awali, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Elisante Fabian licha ya kumuahidi Mkuu wa Mkoa kutoa huduma bora kwa wagonjwa, ameeleza faida za maboresho hayo ni pamoja na kuongeza wigo wa utoaji wa huduma, ongezeko la idadi ya wagonjwa na mapato ya Hospitali, upatikanaji wa vipimo vyote 38 sambamba na kupunguza muda wa kuhudumia mgonjwa.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AUNDA TUME KUFUATILIA SAKATA LA MACHINJIO NGORBOB ARUMERU..

    September 09, 2025
  • WAMAREKANI WATALII KWA WINGI TANZANIA- KAIMU BALOZI MAREKANI TANZANIA..

    September 11, 2025
  • RAIS SAMIA KUZIUNGANISHA MONDULI NA NGORONGORO KWA BARABARA YA LAMI..

    September 10, 2025
  • KILA LA KHERI DARASA LA SABA 2025..

    September 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa