• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WALIOLALAMIKIA MGAO WA MAJI WAFURAHIA UJENZI WA TENKI JIPYA LA MAJI...

Posted on: September 24th, 2025

 *_Latajwa kuondoa changamoto ya Maji kwenye Mtaa wa Kimindorosi, Rc Makalla akipiga marufuku ubambikiaji wa ankara za Maji*_


Wananchi wa Mtaa wa Kimindorosi Kata ya Olasiti Mkoani Arusha wameishukuru serikali kwa hatua za haraka za ujenzi wa Tenki jipya la Maji katika Mtaa wao litakalokuwa na uwezo wa kuhifadhi maji Lita 50,000 na hivyo kuondoa changamoto ya maji kwenye eneo hilo iliyotokana na jiografia ya Mtaa huo kuwa mlimani na hivyo kuathirika na upatikanaji wa maji pale mahitaji yanapokuwa makubwa kwenye maeneo ya tambarare.


Leo Septemba 24, 2025, wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa Mhe. CPA Amos Makalla ya kukagua miundombinu na utoaji wa huduma ya Maji kwa wananchi wa Jiji la Arusha, Mhandisi Justine Rujomba, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira Jiji la Arusha (AUWSA), amemueleka Mkuu wa Mkoa na wananchi hao kuwa tenki hilo jipya la Maji litaanza kujazwa maji usiku wa leo na kuanza kuhudumia wananchi wa eneo hilo na hivyo kumaliza kabisa changamoto ya Maji kwenye Mtaa huo.


Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Kimindorosi Bw. Amani Saruni amesema Mtaa wake umekuwa ukikabiliwa na changamoto ya Maji hasa msimu wa kiangazi kutokana na mahitaji makubwa ya eneo hilo na Jiografia ya Mtaa wake, akisema kujengwa kwa tenki hilo kunaenda kuondoa changamoto ya Maji kwenye Mtaa huo na kutoa hakikisho la Maji ya Uhakika na salama katika vipindi vyote


Awali wakati wa maelekezo yake Mhe. Makalla amebainisha kuwa amejiridhisha na uzalishaji wa maji kwenye Jiji la Arusha, akielekeza wananchi hao kupata maji safi na ya uhakika kama ilivyoahidiwa, akipiga marufuku pia ubambikiaji wa ankara za maji kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha.


"Natoa maelekezo tufanye kazi tuhakikishe maji yamejazwa na kesho maji kwa wananchi iwe bwerere katika eneo hili. Hili tenki hapa ni kwaajili yenu ili kuwapa uhakika wa maji naombeni muendelee kutoa ushirikiano kwa mamlaka ya Maji na kutunza miundombinu hii ya Maji." Amesema Mhe. Makalla.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA: UFUNGUZI TAWI LA CRDB NAMANGA UTACHOCHEA BIASHARA NA UCHUMI WA WANANCHI WA MPAKANI ..

    September 26, 2025
  • RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027...

    September 25, 2025
  • WANANCHI WALIOLALAMIKIA MGAO WA MAJI WAFURAHIA UJENZI WA TENKI JIPYA LA MAJI...

    September 24, 2025
  • RC MAKALLA: ARUSHA ITAENDELEA KUWA NA AMANI SASA NA HATA  BAADA YA UCHAGUZI...

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa