• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZAZI KUWENI MAKINI MNAPOWAHAMISHA WATOTO WENU

Posted on: December 10th, 2019

Wazazi watakiwa kuwa makini  na udanganyifu hasa katika kipindi cha kufanya uhamisho wa watoto wao waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2020.

Yamesemwa hayo na katibu tawala wa Mkoa wa Arusha bwana Richard Kwitega alipokuwa akitangaza rasmi uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2020 kwa mkoa wa Arusha.

“Kuna watu wanatabia ya kuwadanganya wazazi watawasaidia kupata shule wanazoziitaji kirahisi kwa ajili ya watoto wao, lakini ukweli na taratibu zilizopo ni, mzazi mwenyewe ndio anatakiwa kuanzia katika ngazi ya shule aliyopangiwa mtoto wake kisha atapatiwa kibari katika ngazi ya halmashauri”,alisema Kwitega.

Amesisitiza zaidi kama uhamisho ni wa shule zilizopo ndani ya halmashauri basi mzazi haitaji kufika katika ngazi ya Mkoa ila kama niwakutoka halmashauri moja kwenda nyingine ndio mzazi atatakiwa kumalizia hatua zote katika ngazi ya Mkoa.

Kwitega amewataka wazazi pia kusubiri mpaka shule zikifunguliwa na wanafunzi wote wamewasili mashuleni ndio taratibu za uhamisho zianze kwani kwa kufanya hivyo itasaidia halmashauri husika kufahamu shule gani zina upungufu na zipi zimejitosheleza.

Akitoa taarifa ya ufaulu wa wanafunzi  wa kujiunga na kidato cha kwanza  afisa elimu Mkoa wa Arusha bwana Halifan Masukila, amesema jumla ya wanafunzi 37,655 ndio waliofanya mtihani kwa mwaka 2019 na kati yao wanafunzi 34,509 ndio walifaulu sawa na asilimia 91.67.

Ambapo wakiume walikuwa 16,573 na wakike 16,636 na hivyo kufanya idadi kubwa ya watahiniwa wa kike kufanya vizuri zaidi ya watahiniwa wa kiume.

Bwana Masuka amesema ufaulu kwa mkoa wa Arusha umepanda ukilinganisha na mwaka jana ambapo ufauli ulikuwa  wa asilimia 87.30 na kuufanya Mkoa kushika nafasi ya pili kitaifa ikiufuatia mkoa wa Dar es Salaam.

Kwa mwaka 2020 jumla ya wanafunzi 29,770 wameshapangiwa shule kwa ajili ya masomo yatakayoonza mapema Januari 2020 na wanafunzi 4,739 wamepangiwa shule lakini wanasubiri ukamilifu wa miundo mbinu katika shule hizo hasa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo.

Hivyo amewataka wazazi kuwa nasubira hasa kwa wale wanafunzi wanaosubiri ujenzi wa miundombuni kikamilika katika shule walizopangiwa.

Mkoa wa Arusha unaendelea kufanya vizuri zaidi katika sekta ya elimu na hii inatokana na utaratibu uliowekwa na uongozi wa Mkoa wa kuhakikisha elimu inakuwa kwa kasi sana ikiwemo ufanyaji wa mtihani mmoja kwa shule zote za Mkoa na hii inasaidia kuweza kupima kiwango cha ufundishaji kwa walimu na kuwapa motisha zaidi pale wanapofanya vizuri.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa