• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

ELIMU YA LISHE IKATOLEWE KATIKA NGAZI ZOTE

Posted on: February 23rd, 2023

Waratibu wa lishe ngazi ya Mkoa na Halmshauri Mkoani Arusha wametakiwa kwenda kutoa elimu ya lishe katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye nyumba za Ibada, mashuleni,minadani na kwenye kamati za lishe za Kata.

Hayo yamesemwa na  Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella alipokuwa akizungumza na Kamati ya lishe Mkoa wakati wa kikao kazi cha tathimini ya lishe ngazi ya Mkoa.

Mongella amesema kuwa tathimini inayofanyika katika viashiria vya lishe haitoshi kujitathimini  na kujihakikishia kuwa elimu ya lishe inayotolewa imewafikia wananchi kwa kiwango kikubwa,bali mikakati madhubuti inatakiwa ijengwe mpaka kwenye Kaya kwa kuhakikisha kila mzazi ananatambua umuhimu wa lishe kwa familia.

Katika kusisitiza hilo amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kwenda kusimamia agenda ya lishe kwa umakini ikiwemo kuhakikisha vikao katika ngazi zao vinafanyika kwa wakati na Wananchi wanapata uelewa wa kutosha kuhusu faida ya lishe wa Jamii.

"Ndugu zangu suala la lishe tusifanye nalo mchezo, lina mchango mkubwa sana katika maendeleo ya Nchi,lishe bora ndiyo inayochangia ustawi wa afya ya mwili na akili kwa watu wetu kwani ndipo wanapopatikana wataalamu mbalimbali katika sekta zote." Alisema Mongella

Akichangia mjadala huo,Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru  James Chembe amesema katika kushughulikia suala la lishe ni vyema wataalamu kama maafisa Kilimo na Mifugo wakashirikishwa kwenye mpango kazi kwani kada zao zina mchango mkubwa katika masuala ya lishe bora.

"Hapo zamani tulikuwa tuna utaratibu kwa kila Kaya kuwa na bustani za mbogamboga na kuwa Mifugo ambayo ilisaidia upatikanaji wa vyakula vya lishe na maziwa,nashauri kurudishwe utaratibu wa kulima bustani katika shule zetu ili wanafunzi waweze kupata chakula bora wakiwa majumbani na shuleni.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Arusha, Sulemani Msumi amesema kuna haja ya kutungwa sheria itakayowabana wazazi ambao watakaidi kuchangia fedha za chakula katika shule ili wanafunzi waweze kupata chakula cha mchana kwani hii itasaidia kupunguza wimbi la watoto wengi kukosa chakula shuleni.

Kikao cha Tathimini ya afua za lishe ngazi ya Mkoa kimejumuisha robo ya kwanza naya pili katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.