• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

POLISI WAPATIWA MBINU KUKABILIANA NA MAUAJI YA WANYAMAPORI BARABARANI..

Posted on: November 9th, 2024

POLISI WAPATIWA MBINU KUKABILIANA NA MAUAJI YA WANYAMAPORI BARABARANI.

Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi

Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Longido Mkoani Arusha leo wamekutanishwa na wadau wa wanyamapori kufundishwa na kujadili kwa pamoja namna bora ya kukabiliana na mauaji ya wanyamapori kwa kugongwa na vyombo vya moto barabarani.

Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Peter Lusesa amesema kutokana umuhimu wa sekta ya Utalii, Jeshi la Polisi lilianzisha mradi unaojulikana ‘Utalii Salama’ ambapo wanyamapori ni mhimili wa sekta hiyo hivyo wanalojukumu la kuhakikisha usalama wa wanyama hao unakuwepo wakati wote.

ACP Lusesa amewataka Askari hao ambao ni Wakaguzi kata pamoja na wale wa usalama barabarani kutumia Mradi huo kwenda kukutana na madereva pamoja na wananchi kwa ajili ya kuwapa elimu juu ya madhara ya kugonga wanyamapori hao lakini pia kuwaeleza faida ipatikanayo kupitia utalii.

Naye Afisa Ikolojia na Utafiti toka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya OIKOS Afrika Mashariki Bi. Eliengerasia Koka amebainisha wameamua kuandaa semina hiyo mahususi kwa ajili ya Askari hususani wale wa kata ili waende kuwaelimisha wananchi kuhusiana na madhara ya kuua au kugonga wanyamapori na faida zao.

Afisa huyo amesema taasisi hiyo imebaini kuwa wanyamapori wengi wanakufa kwa kugongwa na magari barabarani hususani katika barabara ya Arusha Namanga na hata zile zinazopita katika vijiji mbalimbali katika wilaya hiyo, hivyo kupitia semina hiyo Askari kata hao watapata maarifa zaidi ya kwenda kuwaelimisha wananchi.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Polisi Wilaya ya Longido Mrakibu wa Polisi SP Juma Bonza amesema endapo wananchi watapewa elimu ya kutosha, kuweka alama za barabarani katika maeneo yenye wanyama wengi pamoja na kuchukua hatua kwa madereva watakaokiuka Sheria itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo hilo.

Naye Mkaguzi Kata ya Namanga Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Zainabu Sengasu amesema elimu waliyoipata wataenda kuifikisha kwa wananchi ambapo amewaomba wadau kufadhili mabonanza kama vile michezo ambayo hukutanisha watu wengi katika kata zao hali ambayo itasaidia kufikisha ujumbe kwa watu wengi zaidi.

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.