• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC MAKONDA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA MADARAJA YA KING’ORI BARABARA YA ARUSHA – MOSHI

Posted on: May 20th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, leo asubuhi amefanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa madaraja mawili ya King’ori yanayojengwa katika barabara kuu ya Arusha – Moshi na kuridhishwa na kasi na ubora wa ujenzi wa madaraja hayo ambayo ni kiunganishi muhimu kati ya mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.



Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Makonda amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za serikali katika kuboresha miundombinu ya usafiri nchini, hasa maeneo ambayo yamekuwa na changamoto kubwa wakati wa mvua ambapo serikali imechukua hatua hiyo baada ya wananchi kadhaa kupoteza maisha katika eneo hilo mwaka uliopita kutokana na changamoto za miundombinu hafifu.



"Serikali ina wajibu wa kulinda maisha ya wananchi wake, ndiyo maana tumetafuta suluhu ya kudumu kwa kujenga daraja imara badala ya makalvati yaliyokuwa yakisababisha madhara na hii ni hatua kubwa ya maendeleo katika kuhakikisha usalama wa barabara hii muhimu.” Amesema Mhe. Makonda.



Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara nchini inaboreshwa na kuwa salama wakati wote – iwe ni kipindi cha mvua au kiangazi pamoja na kuipongeza Wizara ya Ujenzi na taasisi husika kwa kutekeleza kwa ufanisi maelekezo ya Mhe. Rais.



Hata hivyo, mesisitiza umuhimu wa watumiaji wa barabara kufuata sheria na taratibu za usalama barabarani ili miundombinu hii iweze kudumu kwa muda mrefu, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hii inapita magari makubwa ya mizigo na pia hutumiwa na watalii wengi wanaotembelea maeneo ya kitalii ya Kaskazini mwa Tanzania.



“Natoa wito kwa wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Mhepp Rais. Badala ya maneno, tuongeze bidii ya kufanya kazi na kutafuta fedha halali. Hii ndiyo njia ya kweli ya kuleta maendeleo ya kweli kwa taifa letu,” ameongeza.



Mradi huo unatekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kqa gharama ya shilingi bilioni 4.6 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 2, 2025.


Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • KARIBU ARUSHA Mhe. KENAN LABAN KIHONGOSI MKUU WA MKOA WA ARUSHA

    June 26, 2025
  • KARIBU ARUSHA Mhe. KENAN LABAN KIHONGOSI MKUU WA MKOA WA ARUSHA

    June 26, 2025
  • SIKU YA KWANZA; WAKAZI WA ARUSHA WAJITOKEZA KWENYE KAMBI YA MADAKTARI BINGWA NA MABINGWA WABOBEZI

    June 23, 2025
  • RC MAKONDA ASHIRIKI MARATHON YA KKKT 2025

    June 21, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.