• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC MAKONDA NA RAIS WA TFF WATETA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YAMWANAMKE DUNIANI

Posted on: February 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, amekutana na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, kujadili maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani leo tarehe 10 Februari, 2025.



Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye `Ofisi ya Mkuu huyo wa Mkoa, viongozi hao wamekubaliana kuweka msisitizo mkubwa katika michezo kama sehemu ya kuadhimisha siku hiyo muhimu ikiwemo kuandaa mashindano ya mpira wa miguu kwa wanawake, ambapo timu nne za wanawake zitashiriki, zikiwemo Simba Queens, Yanga Queens, JKT Queens na Fountain Gate FC.



Aidha, Viongozi hao wamekubaliana kawa, TFF itaweka banda maalum katika maadhimisho hayo ili kutoa elimu kuhusu maendeleo ya soka la wanawake na kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika michezo mbalimbali.



Mbali na michezo, maadhimisho hayo yataambatana na Wiki ya Utoaji wa Huduma kwa Wanawake, ambapo sekta mbalimbali zinazohusiana na maendeleo ya wanawake zitashiriki kutoa huduma na elimu kwa wananchi wa Arusha na maeneo ya jirani.



Hata hivyo, Mhe. Paul Makonda  amesisitiza kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuinua hadhi ya mwanamke katika nyanja mbalimbali, hususan michezo, afya, elimu na uchumi na kuwataka wadau mbalimbali kushirikiana kwa karibu kuhakikisha hafla hiyo inafanikiwa na kuleta matokeo chanya kwa jamii.



Kwa upande wake, Rais wa TFF, Wallace Karia, ameahidi kuwa shirikisho hilo litaendelea kuwekeza katika maendeleo ya soka la wanawake na kushirikiana na serikali na wadau wengine kuhakikisha mpira wa miguu kwa wanawake unapata msukumo unaostahili.



Maandalizi ya maadhimisho hayo yanaendelea, na wananchi wa Arusha wanatarajiwa kushiriki kwa wingi katika hafla hiyo ambayo itaadhimishwa Kitaifa 08 Machi, 2025 Mkoani Arusha.


Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.