• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAKOGA NYOYO ZA WALIMU ARUSHA....

Posted on: November 19th, 2023

Na Elinipa Lupembe.

Kufuatia mkakati wa Serikali ya awamu ya sita ya kuboresha miundombinu katika sekta ya elimu, kupitia program ya kuboresha miundombinu ya shule za Sekondari nchini (SEQUIP), mpango unaoenda sambamba na ujenzi wa nyumba za walimu, umewagusa na kukoga nyoyo za walimu kwa kuona Serikali inawajali.

Wakizungumza na mwandishi wetu, Walimu wa shule ya Sekondari Kiutu, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha, wamethibitisha kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imekoga nyoyo za walimu nchini, kwa kuweka mazingira wezeshi  wanayowapa unafuu katika tendo na kufundisha na kujifunza shuleni.


Wamesema kuwa tofauti na hapo awali, Serikali iliwekeza zaidi, katika kuimarisha miundombinu ya wanafunzi na kuwaachwa walimu, jambo ambalo liliwapa wakati mgumu katika ufundishaji lakini Serikali ya Awamu ya Sita imeenda mbali zaidi kwa kuwajali wanafunzi na walimu pia.


"Tendo la kujifunza na kufundisha linakwenda pamoja unapomuacha mmoja kati yao nyuma, inakuwa ni ngumu kufikia malengo ya uhamishaji wa maarifa kati ya mwalimu na mwanafunzi, unatengeneza uwazi 'gape',tunachelea kusema Serikali imetutendea haki walimu" Wamesema walimu hao


Mw. Fedrick Komba, amesema kuwa, shule ya sekondari Kiutu, ni shule mpya imejengwa majengo yote ya shule pamoja na nyumba ya walimu yenye sehemu za kuishi familia mbili, jambo ambalo wanaamini litaongeza tija katika ufundishaji na kupandisha kiwango cha taaluma kwa wanafunzi..


Naye mwalimu wa Taaluma sekondari Kiutu, Mwl. Stanley Antony Mwampimbe,  amesema kuwa kuwepo kwa nyumba nzuri za walimu zinawapunguzia makali ya maisha kwa kulipa kodi pale wanapoishi nyuma za kupanga, wanatumia gharama kubwa kulipa kodi za nyumba..


"Hapa Arusha gharama za maisha ziko juu na kusababisha kodi za nyumba kuwa juu pia, uwepo wa nyumba za walimu zinatupunguzia makali ya maisha, kwa serikali kutupunguzia mzigo wa kulipa kodi, walimu wa sasa tunaweza kuwa na maisha mazuri kama watumishi wengine wa Umma" Ameweka wazi Mwl. Mwampimbe.


Awali serikali kupitia mpango wa SEQUIP imejengea nyumba ya walimu yenye sehemu ya kuishi familia mbili (2in1), kwa shilingi milioni 98, shule ya sekondari Kiutu, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 -2025.


Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.