• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

SERIKALI YAJA NA MFUMO WA KUSAJILI VITAMBULISHO VYA MACHINGA KIDIGITALI.

Posted on: February 19th, 2024


Kufuatia mkakati wa Serikali wa Kuwasajili Wajasiriamali maarufu kama machinga Kidigitali, imeanza kutoa mafunzo kwa Maafisa TEHAMA, Maendeleo ya Jamii na Biashara kutoka halmashauri za Mkoa wa Arusha, ili waanze kuwasajilijili wafanyabiashara hao wadogo.


Mfumo huo utakaowezesha wajasiriamali wote, kutambuliwa, kusajiliwa na kupata Vitambulisho vya Kidijitali vitakavyowawezesha kutambulika rasmi na kunufaika na fursa za kibiashara zilizopo.


Akifungua Mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Missaile Albano Musa, Katibu Tawala Msaidizi, Mipango na Uratibu, Apolinary Seiya, amewataka Maafisa hao kufuatilia kikamilifu mafunzo hayo ili kupata ujuzi na maarifa yatakayowawezesha kufanya zoezi hilo la kitaifa kwa weledi mkubwa na kufikia malengo ya Serikali ya kuwatambua wajasiriamali rasmi kwenye mfumo wa kidijitali iliyoainishwa.


Amesema kuwa, mafunzo hayo ni utekelezaji wa adhima ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wajasiriamali kutambulika rasmi ili waweze kunufaika na fursa rasmi zinazotolewa na Serikali kupitia taasisi za kifedha kama vile mikopo yenye riba nafuu.


"Mfumo wa Utambuzi na usajili wa kutoa vitambulisho kwa wafanyabiashara ndogondogo umekamilika baada ya kufanyiwa maboresho makubwa ili uweze kupata vitambulisho vya kidigitali, niwatake sasa mkafanye zoezi hili kwa weledi mkubwa katika maeneo yenu bila kutoa upendeleo kwa mfanyabiashara yeyote." Amesema Seiya


Mfumo wa utambuzi, Usajili na utaoji wa vitambulisho utawezesha kuwatambua, kuwasajili na kuwapa vitambulisho vilivyounganishwa na mfumo wa NIDA, vitambulisho ambavyo vitawapa fursa ya wajasiriamali ya kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka taasisi za fedha.


Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Juliana Mtolela amesema kuwa, vitambulisho hivyo vitakuwa tofauti na vile vya zamani kwani vitakuwa vya kidigitali na vitakuwa na taarifa zote za muhimu za mfanyabiashara zikiwa zimeunganishwa na taarifa za vitambulisho vya NIDA na kumfanya kutambulika rasmi na Serikali pamoja na Taasisi zingine za kifedha.


Hata hivyo, washiriki wa mafunzo hayo wamethibisha kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka yanayokwenda kuwezesha kutambua mahitaji ya wajasiriamali  na kutafuta namna bora ya kuwahudumia.


"Tunashukuru sana Serikali kuwezesha mafunzo haya kufanyika, yatatusaidia kupata takwimu sahihi ya wajasiriamali na wamachinga kwaajili ya kuwa na njia sahihi ya kutatua changamoto zinazowakabili sambamba na wao kunufaika na fursa mbalimbali za mikopo kutoak taasisi za fedh." Amesema Afisa Bishara Wilaya ya Monduli, Edna Fransis.


Ikumbukwe kuwa, mafunzo hayo ya mfumo huo ni ahadi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa 25 Januari, 2022 ya kuunda mfumo rasmi wa  kuwatambua wajasiriamali  wadogo Kidigitali ili watambulike katika mfumo rasmi.


#arushafursalukuki



Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.