• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

SERIKALI YATIMIZA AHADI, YAANZA KUTOA VITAMBULISHO VYA NIDA, KWA WALIOJIANDIKISHA ARUSHA....

Posted on: December 1st, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, imetimzia ahadi yake wka wananchi, kwa kuanza kutoa vitambulisho vya Taifa, maarufu kama NIDA, kwa wananchi waliojianzikiwasha nchini, mkoa wa Arusha ukiwa miongoni mwao, zoezi ambalo lilikwama kwa zaidi ya miaka minne sasa.


Akizungumza wakati wa akizindua zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya NIDA kimkoa, wilayani Karatu, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K.Mongella, amesema kuwa, Serikali imekamilisha ahadi yake kwa wananchi  waliojiandikisha kwa kuanza kuwagawia vitambulisho vyao vya taifa huku akiwahakikishia wakazi wa mkoa huo kuwa, kila mwananchi mwenye sifa atapata kitambulisho cha Taifa.


Amesema kuwa, takribani watu 931,221, waliojiandikisha mkoani hapo, watapata vitambulisho, na tayari vitambulisho 880,000 vimeshafika kwenye ofisi za NIDA wilaya zote za mkoa huo, tayari kugawanywa kwa wananchi.


Leo nimekabidhi vitambulisho 99,132 kwa Maafisa Watendaji wa kata za Wilaya ya Karatu, ili wakawakabidhi Watendaji wa vijiji na viwafikie wananchi kwenye maeneo yao.


Aidha amewaagiza Maafisa Watendaji, kuhakikisha vitambulisho hivyo vinagawiwa kwa walengwa ndani ya siku 14, na kwa waliofariki dunia vitambulisho visitolewe, bali virejeshwe Ofisi za NIDA za wilaya.


"Rai yangu kwa Watendaji wote, kila kitambulisho akabidhiwe mhusika mwenyewe, kusitokee ubabaishaji wowote, kwa mtu aliyefariki rudisheni taarifa zake NIDA, asikabidhiwe kitambulisho mtu asiyehusika"Ameweka wazi


Amesisitiza wananchi wenye sifa, kuona umuhimu wa kuwa  na kitambulisho cha Taifa, kwa kuwa mwelekeo wa Serikali sasa, ni kuingiza taarifa za kila mtanzania kwenye mfumo wa kidijitali, ambao utarahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa kila mtanzania.


Hata hivyo wananchi wa Karatu wameishukuru Serikali, kupitia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa vitambulisho vyao, ambavyo wamekuwa wakivisubiri kwa muda mrefu huku wakipata usumbufu mkubwa, ikiwemo kukosa baadhi ya huduma zilizohitaji kuwa na kitambulisho hicho.


Bupe Alfred Mwankusye, mkazi na mjasiriamali wa Karatu mjini, ameweka wazi kuwa, licha ya kuishukuru Serikali kwa kuwakabidhi vitambulisho vyao na kuongeza kuwa, kutokuwa na vitambukisho vya NIDA, walikwama kwenye masuala ya mikopo kutoka Taasisi za fedha ambazo zililazimu kuwa na kitambulisho hicho


"Tunamshukuru mama Samia kwa kutupa vitambulisho, wananchi tuliteseka, hasa wajasiriamali tulipohitaji kuchukua mikopo ya kuendeleza biashara, kwa sasa mambo yetu yatakwenda kama tunavyopanga" Amesema Mwajabu Khasim,


"Tulipia changamoto nyingi, kuna wakati  nilimpeleka mtoto shule, nikapata usumbufu sana kwa kutokuwa na kitambulisho cha NIDA kwa sasa tunasema Kazi iendelee". Martina Philipo.


Ikumbukwe kuwa, ugawaji wa vitambulisho vya Taifa kwa watanzania, ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020 - 2025


#ArushaFursaLukuki

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.