• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

TAWTO WAKARABATI JENGO LA OFISI YA POLISI DAWATI LA JINSIA ARUSHA.

Posted on: February 13th, 2024


Chama cha wanawake Mawakala wa Utalii Tanzania (TAWTO) wamekarabati Jengo la Ofisi ya Polisi Masuala ya Jinsia na watoto, Wilaya ya Arusha na Kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella.


Jengo hilo, lililokuwa uchakavu kutokana na kujengwa kwa muda mrefu, lilepambwa kwa michoro inayovutia ya wahanga wanaofanyiwa ukatili kueleza zaidi changamoto wanazokumbana nazo kwenye jamii pamoja na kuwekwa samani za ofisi.


Akikabidhi jengo hilo Jijini Arusha, Mwenyekiti wa TAWTO, Elizabeth Ayo amesema chama hicho kimeona umuhimu wa kukarabati jengo la Dawati hilo, litakalosaidia katika kusimamia na kulinda haki za wanawake na watoto pamoja na watoa huduma ambao ni Jeshi la Polisi.


"Tumeamua kuunga mkono juhudi za Serikali kwa fedha kidogo tuliyojaliwa kama chama ili jamii hususani wanawake na watoto waweze kupata haki kwenye mazingira rafiki kwa wahusika". Amesema.


Akizungumza wakati akikabidhiwa jingo hilo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. JOHN V.K Mongella, amewashukuru wadau hao kwa kujitolea kusadia kuboresha mazingira ya utoaji huduma kwa jamii kupitia Dawati hilo la Jinsia kwani wanafanya mambo makubwa katika kuhakikisha uchumi wa nchi unakua kupitia sekta ya utalii.


"Hiki mlichofanya Mungu atawalipa sababu kuna watu wanataabika na unyanyasaji ikiwemo ukatili kwa watoto, wanawake na wanaume ambapo sasa ukarabati huu utatoa ari zaidi katika kutafuta suluhu ya changamoto za ukatili ikiwemo kulinda haki za watoto na kinamama".


Hata hivyo Mhe. Mongella ametoa rai kwa wananchi wote kutojihusisha na vitendo vya kikatili kwa makundi yote na kusababisha madhara ya kisaikolojia kwani hatua za kisheria zitaendelea kufuata mkondo wake ili kudhibiti matukio hayo huku akitoa wito kwa wadau wa maendeleo kuiga mfano wa Taasisi hiyo kwa kujitokeza na kutoa michango yao kusaidia jamii.


Akisoma taarifa fupi, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi ambaye ni Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Arusha, Ursula Mosha amesema dawati  la Jinsia na watoto ni dawati lenye kusaidia jamii kuhusu kupinga unyanyasaji wa kijinsia wanaofanyiwa wanawake, watoto na wanaume ambapo Awali dawati hilo lilianzishwa mwaka 2010 kwa kuhudumia jamii na kushauri dhidi ya ukatili.


Amesema kuwa dawati hilo linatoa  huduma ya ushauri kwa wanandoa ikiwemo elimu na makuzi, kuunganisha familia zilizotengana pamoja, ushauri wa usiri kwa wahanga wa ukatili katika Dawati la Jinsia la Huduma kwa Pamoja lililopo Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru ikiwemo utoaji wa elimu kwa jamii.


Pia Alishukuru TAWTO kwa kusaidia ukarabati wa jengo hilo lililokuwa chakavu kwa kupewa meza tano za kisasa,viti kumi na mabenchi matatu ikiwemo marekebisho ya upakaji rangi,paa sakafu ikiwemo michoro ya kuhamasisha watoto wanapofika dawati kutoa changamoto zao za ukatili.


"Tunalengo la kuwa na jengo huru ili kutoa uhuru kwa wahanga wanaofanyiwa ukatili na pia michoro itakapokamilika tunawaomba wadau wajitokeze zaidi kuchangia dawati hilo tunawashukuru sana TAWTO kwaukarabati huu"


Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.