• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

WATANZANIA TUJIAMINI TUNAWEZA KUFANYA MAMBO MAKUBWA-RAIS MAGUFULI

Posted on: October 24th, 2020

Zaidi ya mabehewa 800 ya mizigo kununuliwa yakiwemo yenye majokofu ili kurahisisha usafirishaji wa maua na mbogamboga ndani na nje ya nchi.

Ahadi hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizundua rasmi usafiri wa treni kutoka Dar es Salaam hadi Arusha kupitia Tanga na Kilimanjaro, katika stesheni za Reli Jijini Arusha.

Amesema wakulima wakubwa wa maua na mbogamboga wapo katika Mkoa wa Arusha hivyo atawarahisishia wafanyabiashara hao katika kupata soko la ndani na nje kupitia reli hiyo.

Amesisitiza zaidi katika maboresho ya huduma za reli nchini, serikali yake itanunua vyichwa vya treni vipatavyo 36 na mabehewa 37 ya abiria.

Amewataka watanzania kujiamini kuwa wanaweza kufanya mambo makubwa ya maendeleo katika nchi yao,hivyo wailinde na kuitunza reli hiyo ili iweze kuwanufaisha vizazi hadi vizazi.

Rais Magufuli amesema treni hiyo inamanufaa makubwa katika kukuza uchumi wa nchi,kupunguza bei za usafarishaji wa abiria na mizigo na kuokoa muda wa usafirishaji.

Akisoma taarifa ya mradi wa ufufuaji wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Arusha Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Reli Tanzania bwana Masanja Kadogosa, amesema treni hiyo ilisimamisha huduma zake tokea mwaka 1986 na sasa serikali ya awamu ya tano imetumia bilioni 14 kurudisha huduma hiyo katika mikoa hiyo ya Kaskazini.

Kadogosa amesema, tokea huduma hiyo kurejeshwa takribani tani 2600 za mizigo zimeshasafirishwa ndani ya mwezi mmoja na abaria wapatao elfu 55 wameshatumia usafiri huo kutoka Dar es Salaam hadi Arusha.

Aidha, amesema usafiri huo wa treni umelenga kutoa huduma kwa wananchi wote hususani wananchi wa kawaida na wafanyabiashara wadogo, ndio maana na hata bei zake zinakidhi hali ya mtanzania.

Nae Theresia Mollel Mkazi wa Jiji la Arusha, amesema kurejeshwa kwa huduma hizo za treni kwa Mkoa wa Arusha kutawasaidia wao kama wakazi kupunguza gharama za usafiri kutoa Dar es Salaam hadi Arusha na pia itawasaidia kuokoa muda wa kusafiri barabarani.

Theresia ameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kurejesha huduma hiyo ya treni na maendeleo mengine yote yaliyofanywa na awamu hiyo.

Uzinduzi wa treni ya abiria na mizigo Kanda ya Kaskazini umefanywa rasmi baada ya huduma hiyo kuadimika zaidi ya miaka 30 na uzinduzi huo umeshihudiwa na viongozi mbalimbali wa serikali na dini.

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.