• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

AUWSA WAPEWA SIKU TATU, KUBORESHA BARABARA YA MSASANI KATA YA MURIET JIJI LA ARUSHA...

Posted on: November 13th, 2023

AUWSA WAPEWA SIKU TATU, KUBORESHA BARABARA YA MSASANI KATA YA MURIET JIJI LA ARUSHA.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji jiji la Arusha (AUWSA), Mhandisi John Ndetico kurekebisha miundombinu ya barabara ya Msasani kata ya Muriet, Jiji la Arusha, iliyoharibika kufuatia mvua kubwa iliyonyesha, usiku wa kuamkia  13 Novemba 2023.


Imesemekana kuwa, kutokana na kazi ya uwekaji wa miundombinu ya maji taka inayoendelea, iliofanywa  na Mamlaka ya Maji, imesababisha baadhi ya maeneo kutitia na kutengeneza mashimo makubwa  na maji  kuingia na kujaa kwenye makazi ya wananchi wa eneo hilo.


Kufuatia uharibufu huo, Mhe. Mongella ametoa maagizo hayo wakati akitembelea barabara hiyo na kujionea madhara yaliyotokana na mvua kubwa na kumuagiza Kaimu Mkurugenzi huyo kukamilisha kazi hiyo kwa viwango vinavyokubalika kwa muda wa siku tatu.


Amemtaka kushirikiana na Viongozi wa kata hiyo huku akitoa rai kwa wananchi wanaishi maeneo hayo kuchukua tahadhari dhidi ya mvua zinazoendelea kunyesha pamoja na kuwasimamia watoto wasipate madhara kwenye maeneo hayo yaliyoharibika.


"Wazazi na walezi kuweni makini kuangalia watoto wenu wasije kuzama maana barabara zimetitia muwe makini ili maafa mengine yasije tokea"

Naye Mhandisi Ndetico amesema mkandarasi aliyepewa mradi huo,Sinohydro  Corporation Ltd alishamaliza  muda wake hivyo Auwsa itafanyia kazi changamoto hiyo ili tatizo hilo lisiweze kujirudia tena.


Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa maeneo yaliyokumbwa na changamoto hiyo, wameiomba serikali kufuatilia kwa ukaribu na kukagua miradi wanayotekeleza na wakandarasi kabla ya kuikabidhi kwa Serikali na kugundua kasoro kama hizo kabla ya madhara kutokea.


“Hii barabara ilikuwa inatumika vizuri bila  changamoto lakini baada ya AUWSA kuanza kuchimba ndipo changamoto hizi zimeanza kutokea licha ya kumlalamikia mkandarasi aliyekuwa anafanya kazi hii lakini hakutusikiliza”. Amesema Herieth Steven Marunda, Mkazi wa msasani


Naye Mwenyekiti wa  Mtaa wa Msasani, Rashid Chidi, amesema kuwa awali wakati AUWSA wanachimba mifumo wa maji taka  walieleza changamoto ya barabara kuharibika na lakini haikufanyiwa kazi lakini kwakuwa mvua zimenyesha na zimeonyesha  tatizo hilo sasa litafanyiwa kazi kwani barabara zimegeuka mahandaki na wakati mwingine kuhatarisha usalama wa watoto wadogo na watu wazi.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa