• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

DKT. GWAJIMA AZINDUA CHANJO YA UVIKO 19 AWAMU YA PILI

Posted on: December 22nd, 2021

Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima amewahasa wananchi kuchukua tahadhari zote za kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 hasa katika kipindi hiki cha sikukuu.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua mpango harakishi na shirikishi wa utoaji chanjo ya UVIKO 19 awamu ya pili, iliyofanyika Jijini Arusha.

Kuna haja kubwa ya kupambana na huu ugonjwa hasa kwa kujikinga na kuchanja kwani bado kuna ongezeko la wagonjwa kwa sasa.

Takwimu zinaonesha kuwa kati ya wagonjwa 10 wa UVIKO 19 waliolazwa hospitalini saba  hawajachanja na watatu wamechanja.

Vifo vinavyitokana na UVIKO 19 kati ya watu 10 saba hufa kwa kutochanja na watatu huwa wakiwa wamechanja.

Kuna umuhimu mkubwa wa kuchanja kwani ugonjwa huo utakuwa mwepesi, na madhara yake ni madogo kulinganisha na asiye chanja.

Amesema kampeni hiyo ya 2 ya kuhamasisha uchanjaji kwa haraka utasaidia watu kuchanja kwa haraka zaidi kwani ugonjwa wenyewe unasambaa kwa haraka hivyo hakuna budi kwenda kwa haraka pia katika kukabiliana nao.

Kampeni hiyo itakuwa ya mtaa kwa mtaa kwa lengo la kutoa elimu kwa Jamii ili iweze kupata uwelewa zaidi na kufanya maamuzi ya hiari ya kuchanja.

Aidha, Dkt.Gwajima ametaja mikao inayofanya vizuri katika utoaji wa chanjo ni: Ruvuma,Mwanza,Dodoma, Kagera na Mara wakati Mikoa ya Manyara, Njombe, Singida, Iringa na Songwe hakufanya vizuri.

Mpango wa Serikali ni kuchanja kwa asimilia 60 ndipo Taifa litakuwa salama zaidi dhidi ya UVIKO 19, hayo yamesisitizwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya  Prof. Abel Makubi.

Amesema jumla ya watu 28218 walidhibitika kupata maambukizi ya UVIKO 19  na kati yao vifo vilikuwa 739 tokea wimbi la kwanza lilipoingia nchini.

Prof.Makubi amesema mpango huu wa uchanjaji wa awamu ya pili unalengo la kuhakikisha elimu inamilikiwa na wananchi wenyewe na wanaelimishana wenyewe katika Jamii zao.

Aidha, Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe amewahimiza wananchi kuwalinda wazee waliopo Vijijini hasa kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka ili kupunguza vifo visivyo vya lazima.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe John Mongella amesema kwa niaba ya wakuu wa Mikoa yote kuwa wao kama wasimamizi wa Mikoa wapo tayari kulifanya hili zoezi liwe endelevu na lenye hamasa.

Pia, elimu hiyo watahakikisha inafika ngazi za chini kabisa kwani kwakufanya hivyo kutaokoa  maisha ya watu na kuongeza kasi ya maendeleo kwa mtu mmoja hadi kwa nchi.

Uzinduzi wa mpango shirikishi na harakishi wa uchanjaji kwa awamu ya pili umefanyika baada ya mpango wa kwanza kuzinduliwa Jijini Dar es Salaam na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan mnamo mwezi Julai.




Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa