• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI TENGENI FEDHA ZA LISHE

Posted on: December 12th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo amesema bado mkoa unaitaji kujipanga zaidi katika swala nzima la lishe na kuongeza nguvu zaidi katika kutoa elimu katika jamii ili dhana hii iweze kueleweka.

Amewataka wataalamu wa lishe kujipanga zaidi ili kuhakikisha fedha zinatengwa kama ilivyopangwa na elimu inapelekwa kwa wananchi, ameyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha pili cha tathimini ya hali ya lishe cha mkoa kwa mwaka 2019/2020.

“Inashanganza sana kuona baadhi ya halmashauri zinashindwa kutoa fedha kiasi cha shilingi 1000 kwa kila mtoto wakati kwenye bajeti zenu mliziweka,sijui shida iko wapi?’’.

Nae mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Dr. Wedson Sichalwe amesema, mkoa umeweka juhudi katika kushirikisha wadau mbalimbali kama vile viongozi wa dini, viongozi wa kimila na taasisi binafsi ili kuhakikisha elimu ya lishe inafika mbali zaidi.

Amesema kama viongozi wa dini wao wana waumini wakutosha  wakizungumzia maswala haya ya lishe itarahisisha zaidi elimu kuwafikia wengi na viongozi wa kimila hali kadhalika wanajua namna yakutoa elimu hiyo kwa jamii zao wakizingatia mila na desturi za sehemu husika.

Sichalwe amesema pia wadau wa moja moja ambao mkoa unafanya nao kazi pia wanamsaada mkubwa wa kuhakikisha elimu ya lishe na ufanikishaji wa afua zake zinawafikia wananchi kwa urahisi.

Mzee wa kimila hali maarufu kama Laigwanani ,Tobiko Kivuike na Isack Lemsongo wameiyomba serikali kuongeza juhudi zaidi ya utoaji  wa elimu ya lishe,iCHF na afya ya uzazi na mtoto katika jamii za kimasai zaidi kwani wengi wao hawana ufahamu nayo.

Wamesema sababu kubwa katika jamii hizo ni mila na desturi za Kimasai zinawafanya wananchi wengi kutotilia mkazo au kuona umuhimu wa haya mambo.

“Ni vema wataalumu wa afya wakaongezwa katika zahanati za kijiji na wakaajiriwa wataalamu maalumu wakutoa elimu hii ya lishe kuliko kusubiri watalaamu wa mjini wanaokuja mara moja moja”,alisema Tobiko.

Pia walipendekeza  katika utoaji wa elimu ya afya ya uzazi na mtoto wanandoa wote wahusishwe kwani katika jamii za kimasai wanaume wengi hupinga sana maswala ya uzazi wa mpango na hivyo kuwa kikwazo kwa wake zao ambao wanataka kutumia njia hizo.

Kikao cha lishe cha mkoa hufanyika kila baada ya robo mwaka wa fedha ili kutadhimini hali ya lishe katika mkoa na changamoto mbalimbali zinazoikumba sekta hiyo katika kufikisha malengo ya Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa