• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

JUMLA YA WAGONJWA 32,136 WAHUDUMIWA KWENYE KAMBI YA MADAKTARI BINGWA NA WABOBEZI ARUSHA

Posted on: July 2nd, 2024


Na Elinipa Lupembe 


Kufuatia Kiliniki ya matibabu yaliyotolewa bure kwenye kambi ya madaktari Bingwa na mabingwa Wabobezi iliyofanyika kwa siku 7 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha, jumla ya wagonjwa 32, 136  wastani wa wagonjwa 4,598 kwa siku, wamepatiwa huduma za matibabu, vipimo, dawa na vifaa tiba. 



Taarifa hiyo imetolewa na Mganga Mkuu Mkoa wa Arusha Dkt. Charle Mkombachepa, kwa waandishi wa habari wakati wa kufunga rasmi Kambi hiyo Julai 01, 2024 ikiwa ni siku ya nane kati ya siku 7 zilizopangwa kukamilisha kambi hiyo.


Dkt. Mkombachepa amesema kuwa kambi hiyo ilianza tarehe Juni 24 ikiwa na wahudumu wa afya 450, ikiwa na lengo la kuhudumia wagonjwa 7,000 kwa wastani wa wagonjwa 1,000 kwa siku, lakini kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi waliofika kupata huduma kwenyw kambi hiyo ililazimika kuongea watoa huduma na kufikia 550, walioweza kufanikisha kuhudumia wagonjwa hao 32, 136.


Aidha ameainisha wagonjwa hao, 32,136, jumla ya wanawake 19,546 sawa na 60.7, wanaume 12,640 sawa na 39.3 na  watoto 4,616 sawana 14.3, waliweza kupata huduma za matibabu na vipimo ambavyo wananchi wenye kipato cha chini wasingeweza kumudu gharama za vipimo hivyo.


Amefafanua kuwa, pamoja na huduma zilizotolewa za vipimo wagonjwa 20 walipimwa kipimo cha RMI, wagonjwa 180 walifanyiwa kipimo cha CT - Scan, wagonjwa 1,820 walipewa rufaa kwenda hospitali ya Mount Meru ambapo 14 tayari wamefanyiwa pasuaji huku wagonjwa 31 wakiwa kwenye ratiba ya upasuaji, na kuongeza kuwa wagonjwa 170 wamepewa rufaa ya kwenda hospitali nyingine za rufaa wagonjwa 265 JCKI, wagonjwa 69 MOI, wagonjwa 20 Hospitali ya Taifa Muhimbili, wagonjwa 2 Benjamin Mkapa na wagonjwa 2 hospitali ya Mirembe za Dodoma.


Hata hivyo,  Dkt. Mkombachepa amempongeza na kumsukuru mkuu wa mkoa wa Arusha ambaye, kambi hiyo ilikuwa ni maono yake yakiwa na lengo la kutoa hudma za afya bure kwa wananchi wasio na uwezo wa kuoata huduma hizo kutokana na kipato duni na hatimaye utekelezaji wake umezaa matunda mema yaliyorejesha matumaini kwa wagonjwa wengi.


Zaidi amewashukuru wadau wote waliojitoa kwa hali ja mali kukamilisha zoezi hilo muhimu wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuunga mkono kambi hiyo kwa kutoa dawa na vifaa tiba pamoja na kupiga simu ya kuwatia moyo watoa hudumu pamoja na kuwapa pole na kuwafariji wagonjo wote.


Awali, ametoa wito kwa wakazi wa Arusha kuwa, wagonjwa wengi wameonekana kuwa na magonjwa yasiyoambukiza, magonjwa ambayo yanaweza kuepukika kwa kuzingatia taratibu za kiafya ikiwemo kufanya mazoezi, lishe bora, usafi binafsi na usafi wa mazingira, kuepuka ulevi wa kupindukia, uvutaji wa sigara, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kujenga tabia ya kupima afya mara kwa mara.

May be an image of 1 person, newsroom, dais and text

May be an image of 1 person and text

May be an image of 1 person and text

May be an image of one or more people and crowd

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa