• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MALIZENI UJENZI WA MADARASA,VITI, MEZA IFIKAPO DISEMBA

Posted on: December 3rd, 2021

Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Dkt.Athumani Kihamia amezisisitiza Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kuhakikisha ujenzi wa Madarasa na utengenezaji wa Viti, Meza na madawati unakamilika ifikapo Disemba 15,2021.

Maagizo hayo ameyatoa alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa madarasa katika Halmashauri ya Arusha yanayojegwa kwa fedha za tozo za miamala na fedha za mapambano dhidi ya UVIKO 19.

"Itakuwa haina maana kama mkimaliza madarasa kwa wakati bila Viti na Meza, maana wanafunzi hawataweza kuyatumia na maana halisi ya darasa ni liwe na Viti na Meza", alisisitiza.

 Serikali imetoa fedha nyingi kwa lengo la kuondoa changamoto ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga kidato cha kwanza kuchelewa kuanza masomo.

Jukumu letu ni kuhakikisha tunamaliza haya madarasa kwa wakati tuliowekewa kwani Rais Samia Suluhu yeye ameshamaliza kazi yake ya kutoa fedha baada ya kuona kuna changamoto ya wanafunzi wa kidato cha kwanza kuchelewa kuanza masomo.

Katika ziara hiyo, Katibu Tawala amekagua ujenzi wa Madarasa 11 shule ya Sekondari Ilkidinga yaliyogharimu Milioni 220, shule ya Sekondari Kiranyi madarasa 13 yenye thamani ya Milioni 260, shule ya Sekondari Mringa madarasa 10 Milioni 200.

Shule ya Sekondari Lengijave darasa moja la Milioni 20, shule ya Sekondari Oldonyosambu madarasa 2 ya thamani ya Milioni 40, shule ya Sekondari Oldonyowas darasa moja la Milioni 20, shule ya Sekondari Mateves madarasa 3 Milioni 60 na shule ya Sekondari Einot madarasa 4 yenye thamani ya Milioni 120.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha bwana Selemani Msumi amewataka walimu wakuu wa shule za Sekondari za Halmashauri hiyo kuongeza muda wa kusimamia ujenzi wa Madarasa hayo hata nyakati za usiku wafunge taa ili kasi ya ujenzi iongezeka.

Aidha, amewapongeza walimu wa shule hizo kwa ushirikiano waliouwonesha unaopelekea ujenzi wa Madarasa kwenda kwa kasi, hivyo ameomba waendelee na ushirikiano huo ili kufanikisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.

Halmashauri ya Arusha ilipatiwa fedha kiasi cha Bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa 100 ambapo 96 ni madarasa ya Sekondari na manne ni madarasa ya shule shikizi 2, hata hiyo kwa Mkoa mzima wa Arusha fedha kiasi cha Bilioni 8.5 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa  ya shule za Sekondari na shikizi.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa