• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MAMA SAMIA AJENGA SHULE YA WASICHANA LONGIDO KUKABILIANA NA MILA NA DESTURI ZILIZOWANYIMA WASICHANA KUSOMA......

Posted on: January 12th, 2024

Na Elinipa Lupembe.


Kufuatia mkakati wa kupambana na mila na desturi potofu zinazosababisha ndoa za utotoni kwa wasichana wa jamii ya kimaasai, Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 3 za kujenga shule ya sekondari ya wasichana wilaya ya Longido.


Shule hiyo ambayo ni miongoni mwa shule zinazojengwa nchini, mkoa wa Arusha umepata fedha za ujenzi wa shule hiyo maalum kwa wasichan, shule ambayo inakwenda kutatua changamoto ya wasichana waloikuwa wakikosa fursa ya kusoma kutokana na mila na desturi za jamii ya wafugaji.


Akizungumza wakati alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K.Mongella, ameweka wazi kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha watoto wote wanapata haki ya kwenda shule huku kukiwa na msisitizo kwa wasichana wa jamii ya wafugaji, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikosa elimu kutokana na kuozeshwa katika umri mdogo.


Amesema kuwa, Serikali ya Mama Samia, imedhamiria kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu, ambapo jamii kubwa ya wasichana wa kimaasai, nayo imepewa kiapumbele, kupitia ujenzi wa shule hiyo inayotarajiwa kuwa na michepuo ya masomo yote ikiwa ni shule ya bweni.


"Tunamshukuru Mheshiwa Rais, Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaangalia wasichana wa jamii ya Kimasaai kwa jicho la kipekee, ujenzi wa shule hii, utaleta mapinduzi makubwa ya kielimu na kijamii kwa wafugaji". Amesema Mhe. Mongella


Hata hivyo, wananchi wa Jamii ya wafugaji, hawakusita kumshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kwa  kuwajali na kuwajengea shule kubwa, nzuri na ya kisasa, maalum kwa watoto wao wa kike, jambo ambalo wamekiri, hiyo ni neema ya Mungu kwa kuwa, hawakuwahi kuwa na ndoto hiyo.


Mjumbe wa kamati ya Ujenzi wa shule hiyo, Salome Melubo Laizer, amesema kuwa, kutokana na kampeni nyingi za kumkomboa msichana wa jamii ya kimaasai, Serikali imekuja na tiba ya ugonjwa sugu ambao, hata walipotaka kumtibu msichana walikosa wodi ya kumlaza, kwa sasa watoto wao wamepata kimbilio sahihi na salama, watalala shuleni.


"Shule hii ni tiba kwa wasichana wetu, sasa watasoma kama watoto wengine wa kitanzania, kinamama tulitamani wasichana wetu wasome, lakini hatukuwa na mahali pa kuwapeleka, kutokana na mila za kabila letu wengi waliishia kuolewa badala ya kusoma" Amekiri Neema Lasirasi


Mayoni Laiza, amethibitisha umuhimu wa shule hiyo, kwa jamio ya wafugaji, kutokana na kuwa karibu karibu na eneo hili, lakini zaidi shule hiyo ni kubwa ambayo itachukua wanafunzi wengi, ambao awali walikosa nafasi ya masomo kutokana na kutokuwepo na shule karibu.


AwalI, Kaimu Mkuu, wa Idara ya Ujenzi, Hlamashauri ya Longido Mhandishi Grace Siriaki, amefafanua kuwa, shilingi Bilioni 3 zinatumika kujenga, jengo la utawala, vyumba 12 vya madarasa, mabweni 8, nyumba mbili za walimu, ukumni wa mikutano na bwalo la chakula.


#ArushaFursaLukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa