• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

POLISI WAPATIWA MBINU KUKABILIANA NA MAUAJI YA WANYAMAPORI BARABARANI..

Posted on: November 9th, 2024

POLISI WAPATIWA MBINU KUKABILIANA NA MAUAJI YA WANYAMAPORI BARABARANI.

Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi

Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Longido Mkoani Arusha leo wamekutanishwa na wadau wa wanyamapori kufundishwa na kujadili kwa pamoja namna bora ya kukabiliana na mauaji ya wanyamapori kwa kugongwa na vyombo vya moto barabarani.

Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Peter Lusesa amesema kutokana umuhimu wa sekta ya Utalii, Jeshi la Polisi lilianzisha mradi unaojulikana ‘Utalii Salama’ ambapo wanyamapori ni mhimili wa sekta hiyo hivyo wanalojukumu la kuhakikisha usalama wa wanyama hao unakuwepo wakati wote.

ACP Lusesa amewataka Askari hao ambao ni Wakaguzi kata pamoja na wale wa usalama barabarani kutumia Mradi huo kwenda kukutana na madereva pamoja na wananchi kwa ajili ya kuwapa elimu juu ya madhara ya kugonga wanyamapori hao lakini pia kuwaeleza faida ipatikanayo kupitia utalii.

Naye Afisa Ikolojia na Utafiti toka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya OIKOS Afrika Mashariki Bi. Eliengerasia Koka amebainisha wameamua kuandaa semina hiyo mahususi kwa ajili ya Askari hususani wale wa kata ili waende kuwaelimisha wananchi kuhusiana na madhara ya kuua au kugonga wanyamapori na faida zao.

Afisa huyo amesema taasisi hiyo imebaini kuwa wanyamapori wengi wanakufa kwa kugongwa na magari barabarani hususani katika barabara ya Arusha Namanga na hata zile zinazopita katika vijiji mbalimbali katika wilaya hiyo, hivyo kupitia semina hiyo Askari kata hao watapata maarifa zaidi ya kwenda kuwaelimisha wananchi.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Polisi Wilaya ya Longido Mrakibu wa Polisi SP Juma Bonza amesema endapo wananchi watapewa elimu ya kutosha, kuweka alama za barabarani katika maeneo yenye wanyama wengi pamoja na kuchukua hatua kwa madereva watakaokiuka Sheria itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo hilo.

Naye Mkaguzi Kata ya Namanga Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Zainabu Sengasu amesema elimu waliyoipata wataenda kuifikisha kwa wananchi ambapo amewaomba wadau kufadhili mabonanza kama vile michezo ambayo hukutanisha watu wengi katika kata zao hali ambayo itasaidia kufikisha ujumbe kwa watu wengi zaidi.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa