• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

*RC MAKALLA AVIPONGEZA VIWANDA VYA A TO Z NA SUNFLAG KWA UZALISHAJI WA BIDHAA BORA...

Posted on: October 23rd, 2025

 _Asema uwekezaji wao umeongeza fursa za ajira na Mapato ya serikali_


 _Waitangaza Tanzania kupitia Masoko yao ya Asia, Marekani na Ulaya__


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatatu Septemba 29, 2025 ametembelea Viwanda vya A to Z na Sunflag Mkoani Arusha, akiwapongeza kwa uzalishaji wa bidhaa bora pamoja na kutoa fursa za ajira kwa wananchi wengi wa Arusha na hivyo kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na wa Mkoa wa Arusha kwa ujumla.


Mhe. Makalla ameeleza pia kufurahishwa na namna ambavyo Viwanda hivyo vimekuwa mabalozi wazuri wa Tanzania, kwa kuzalisha bidhaa ambazo zimekuwa zikiuzwa ndani na nje ya Tanzania pamoja na kusaidia katika uongezaji wa thamani ya mazao ya kilimo nchini ikiwemo zao la Pamba kutoka Mwanza linalotumika katika utengenezaji wa mavazi kwenye Kiwanda cha Sunflag kilichopo Njiro.


"Nimefika kwenu kwasababu ninyi ni walipaji wazuri wa kodi kwenye rekodi zetu, la pili mmeajiri watu wengi mkiisaidia serikali katika uzalishaji wa ajira kwa Watanzania na Jingine mnaitangaza nchi yetu kwa bidhaa mnazozitengeneza kwenye masoko ya ndani na nje ya Tanzania." Amesisitiza CPA Makalla wakati akizungumza na uongozi na menejimenti ya Viwanda hivyo.


Kulingana na Uongozi wa Viwanda hivyo Kiwanda cha A to Z kimeajiri zaidi ya Watanzania 8,000 huku Sunflag ikiwa imeajiri wafanyakazi 2700 kati yao 43 wakiwa Raia wa Kigeni, wakizalisha Mavazi mbalimbali pamoja na bidhaa za Plastiki na vifungashio mbalimbali ambapo Mhe. Makalla ameahidi kuendelea kushirikiana nao katika kutimiza dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anayehimiza na kufanya jitihada za kuhakikisha Tanzania inakuwa na mazingira bora ya wafanyabiashara na Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuweza kufanya biashara zao katika mazingira mazuri na yaliyo salama.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TAMISEMI YA SAMIA; MAFANIKIO YANAONEKANA...

    October 10, 2025
  • DKT. SAMIA AMEBORESHA VIWANJA VYA NDEGE ARUSHA NA MANYARA KUKUZA UTALII NCHINI- RC MAKALLA...

    October 10, 2025
  • JE WAJUA??? HALI YA UPATIKANAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA MKOA WA ARUSHA WAFIKIA ASILIMIA 93 ..

    October 09, 2025
  • KARATU DC YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA 2025

    October 06, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa