• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA AUNDA TIMU YA KUSHUGHULIKIA KERO ZA WADAU WA SEKTA YA UTALII ARUSHA..

Posted on: April 13th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amekutana na wadau wa sekta ya Utalii mkoa wa Arusha na hatimaye kuunda Timu Maalum, itakayokwenda kushughulikia changamoto zinazoikabili sekta hiyo kwa ujumla wake.

Mhe.  Makonda ameunda timu hiyo mapema leo alipozungumza na wadau hao kwenye kikao, kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano ofisi ya mkuu wa mkoa huo, timu inayojumuisha wadau wa sekta hiyo na Watalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha.

Mhe. Makonda ameiagiza timu hiyo kufanya kazi hiyo ndani ya mwezi mmoja na kuja na maoni na ushauri wa namna bora ya kutatua changamoto zinazowakabili wadau wa sekta hiyo ikiwemo ulipaji wa tozo za serikali na mapato ya Halmashauri.

Amefafanua kuwa lengo la Serikali ya awamu ya Sita inyoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kutengeneza mazingira rafiki kwa wadau na wafanyabiashara wote, waweza kulipa kodi za Serikali bila shuruti na kuendelea kufanya shughuli zao za Kiutalii katika mazingira mazuri.

Hata hivyo, ameitaka Ofisi ya Mkurugenzi wa jiji la Arusha kutumia mifumo ya Serikali katika ukusanyaji wa Mapato ya Serikali ili kupunguza migogoro na wafanyabiashara hao, sambamba na kupunguza gharama za kutumia magari ya Serikali kwenda kukusanya mapato.

“Nendeni sasa mkajikite kutumia mifumo ya kidigitali ambayo imeundwa kurahisisha shughuli za ukusanyaji wa mapato ya Serikali, kuondoa mianya ya rushwa na kupunguza Migogoro na wafanyabiashara.” Amesisitiza Mhe. Makonda.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha watalii Tanzania, Wilbert Chambulo, amezitaja changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ulipaji wa mapato ya halmashauri, hali inayokatisha tamaa ya kuendelea kufanya shughuli zao na wakati mwingine kupelekea uwepo wa mianya ya rushwa kwa baadhi ya wadau.

Naye, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Mhandisi Juma Hamsini, ameahidi kushirikiana na wadau hao kuunda timu hiyo na kushulikia changamoto hizo ndani ya Mwezi Aprili.

Awali, kikao hicho kuwakutanisha pamoja wadau wa sekta ya Utalii na Wataalam wa sekta zote za Umma za mkoa wa Arusha, kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto zinazoikabili sekta hiyo

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa