• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AONGOZA HARAMBEE KANISA LA KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI KATI USHARIKA TARAJALI WA MAGUNGANI JIJINI ARUSHA......

Posted on: October 15th, 2023


Na Elinipa Lupembe.

Mgeni rasmi na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella ameongoza harambee kupata fedha za kiasi cha shilingi milioni 90 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa majengo matatu kwenye kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati Usharika wa Magungani ulioko kata ya Sokoni I Jiji la Arusha.

Akizungumza wakati wa kuongoza Harambee hiyo Mhe. Mongella ameushukuru uongozi wa kanisa kuwa kumualika kufanya kazi hiyo ya kumtumikia Mungu, ambayo amethibithisha na kuahidi kushirikiana nao,mpaka ujenzi huo utakapokamilika na usharika huo tarajali utakapozinduliwa na kuwa usharika kamili.

Amethibitisha kubarikiwa na kushibishwa na neno la Mungu lilohubiriwa lililowakumbusha waumini kujitoa na kuchangia kazi za Mungu na kuongeza kuwa yeye anaamini sadaka inayouma ndiyo sadaka ya kweli.

Aidha amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inatambu na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na madhehebu ya dini, kwa kutekeleza miradi mingi ya kuwahumiwa wananchi wa Tanzania, miradi ambayo kimsingi ingefanywa na serikali.

"Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anasisitiza viongozi wote wa serikali kushirikiana kwa karibu na makanisa na viongozi wa dini, kwa kuwa anathamini mchango unatolewa na Taasisi za dini kusadia jamii ya watanzania husani wenye kipato cha duni" Amesema Mhe. Mongella

Hata hivyo changizo hilo limefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi milioni 13,218,500, ikiwa fedha taslimu milioni 7.4 na ahadi shilingi milioni 5.7 huku milioni 67.7 zikihitajika kufikia mwendo wa milioni 90 uliopangwa.

Katika harambee hiyo Mkuu huyo wa mkoa kwa niaba ya ofisi yake amechangia kiasi shilingi milioni 5 kwa kutao fedha taslimu shilingi milioni 1 na kuahidi kukamilisha shilingi milioni 4 kabla ya tarehe ya uzinduzi wa usharika huo mapema mwezi Novemba 2023

Akiongoza ibaada, Mkuu wa Kanisa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Baba Askofu Dkt. Solomon Massagwa, kupitia neno la Mungu lililogusia suala la imani inayoendana na matendo, amewakumbusha waumini wa kanisa hilo katika harambee hiyo wakumbuke kumtolea Mungu sadaka iliyonona ili kukuza imani kwa wale waisoamini nao wamtukuze Mungu kupitia wao.

"Imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo, na imani inaendana na matendo imani isiyo na matendo, Biblia inasema imani hiyo imekufa, tunapomtolea Mungu leo, tunakamilisha imani zetu kama wakristo hivyo sadaka ya kumjengea Mungu kanisa inambariki Mungu na kuishi kwenye mioyo yetu" Amesema

Akisoma risala ya  Harambee, Mchungaji Kiongozi Usharika Tarajali wa Magungani, Mch. Thomas Kaika amesema lengo la harambee hiyo ni kukusanya shilingi milioni 90 kwa ajili ya kukamilisha jengo la utawala, darasa la shule ya Jumapili pamoja na maliwato za kisasa kwa kuwa kitambo si kirefu usharika huo tarajali utakuwa Usharika Kamili.

"Tayari tulianza ujezi jengo limefikia hatua za kupandisha kuta na mpaka hapo tunahitaji milioni 90 fedha ambazo zitakamilisha ujenzi wa miundombinu pamoja na kuanda shughuli za usimikaji wa Usharika zinazotegemea kufanyika mwezi Novemba 2023" Ameweka wazi Kiongo wa Kanisa

Naye Mwenyekiti wa Changizo Mwl. Lidya Kikura , licha ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya Mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kukubali kushiriki kwenye harambee hiyo ya upanuzi wa miundombinu ya kanisa, amewashukuru pia washarika wote kwa kujitoa kwa hali na Mali bila kujali hali maisha, kipato na uchumi wao na kuwaomba kuendelea kuzoa Baraka hizo kwa Mungu kupitia matoleo yao.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Changizo Mwl. Lidya Kikura , licha ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya Mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kukubali kushiriki kwenye harambee hiyo ya upanuzi wa miundombinu ya kanisa, amewashukuru pia washarika wote kwa kujitoa kwa hali na Mali bila kujali hali maisha, kipato na uchumi wao na kuwaomba kuendelea kuzoa Baraka hizo kwa Mungu kupitia mayoleo yao

#arushafursalukuki
#KaziInaendelea










Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa